Thursday, February 16, 2012

Somo la 7: Bwana wa Sabato

Somo limetafsiriwa na Mgune Masatu

(Mwanzo 2, Kutoka 20, Kumbukumbu la Torati 5, Marko 15)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: Juma lililopita tulijadiliana kwamba sheria ya Mungu inadhamiria kuwa mbaraka kwa wanadamu, sio kitu cha kutufanya tujikwae. Mojawapo ya mbaraka mkubwa wa sheria ni Sabato. Nilipokuwa kwenye shule ya sheria, mpambano ulikuwa mkali. Sio tu kuwa shule ya sheria ilihitajika mtu kusoma kwa bidii, bali pia wanafunzi walifahamu kuwa ubora wa kazi ambayo wangeipata baada ya kumaliza masomo ya shule ya sheria ulitegemea na nafasi yao kimasomo darasani. Baada ya kumaliza mwaka wa kwanza, shule ilikabiliana na shinikizo kubwa kwa kutotoa matokeo kulingana na nafasi aliyoishika mwanafunzi darasani! Nilikuwa na mahala pangu salama pa kujihifadhi, Sabato. Katika siku hiyo sikufanya kazi yoyote ya shule – na niliweza kupata pumziko bila kujisikia hatia! Kwa hakika nilijisikia vizuri sana. Mungu alibariki uaminifu wangu na akanipatia alama nzuri sana. Hetu tuzame kwenye somo letu la Biblia na tujifunze zaidi kuhusu Sabato.

I. Alama za Sabato

A. Soma Mwanzo 2:1-3. Hapo awali tulijadili mafungu haya kwenye somo letu lililohusu utakatifu wa Mungu. Je, tulisema kitu gani kuhusiana na Sabato kuwa takatifu? (Kuwa takatifu ilimaanisha kuwa iliwekwa wakfu kinyume na siku nyingine zote. Ilibarikiwa. Utakatifu wake ulitokana na kitu kilichofanywa na Mungu, sio kitu chochote tulichokifanya sisi.)

B. Soma Marko 2:27. Je, unadhani ni kwa nini Mungu aliifanya Sabato? (Ilifanywa kwa ajili yetu. Kimsingi, ilifanywa kuwa siku ya pumziko kwa ajili yetu.)

C. Soma Kutoka 20:8-11. Je, ni sababu gani nyingine tunayoiona kwa Mungu kuifanya Sabato kuwa takatifu? (Ukumbusho wa uumbaji wa Mungu wa “mbingu na nchi.”)

D. Soma Kumbukumbu la Torati 5:12-15. Je, ni sababu gani tunayoiona hapa ya kuitunza Sabato? (Mungu aliwaokoa watu wake kutoka kwenye kutendewa kusikokuwa kwa haki. Kwa hiyo tunapaswa kuwatendea wale walio chini yetu mambo ya haki kwa kuwapatia pumziko la Sabato.)

1. Je, hiyo ndio sababu ya kutufanya tuamini kuwa Sabato ilifanywa kwa ajili ya Wayahudi pekee? (Hapana. Ulikuwa tu ni mfano wa “kuokoa.” Mungu aliingilia kati ili kuweza kuleta haki. Hivi leo Mungu anatuokoa kutoka kuwa watumwa wa dhambi na kifo.)

II. Sabato Inayofananishwa na Mpira wa Kimarekani

A. Soma Marko 15:33-34, Marko 15:37-39 na Marko 15:42-43. Je, Yesu alisulubiwa siku gani? (Ijumaa, kabla ya Sabato.)

B. Soma Marko 16:1-3 na Marko 16:5-9. Je, Yesu alifufuka kutoka kaburini siku gani? (Jumapili.)


1. Kwa nini ucheleweshaji huu? Hebu jiweke kwenye nafasi ya Mungu Baba. Ni punde tu Mwanao amepigwa hadi mauti kumkuta. Kabla Mwanao hajafa anakwambia, “Kwa nini umeniacha?” Kwa kuongezea, ni punde tu Mwanao ameshinda “Mpira wa Kimarekani (American Football)” wa hapa duniani – ameishinda dhambi na kuuleta ushindi katika Ufalme. Je, utachukua muda gani kumkumbatia Mwanao? Je, utachukua muda gani kusema, “Sijakuacha!” (Sitasubiri! Kwa hakika kabisa, sitasubiri.)

a. Je, kwa nini Mungu alifanya kile ambacho hakuna hata mtu mmoja angeweza kukifanya? (Mungu alisubiria kwa sababu ile ile ambayo alisherehekea uumbaji wa dunia katika siku ya Sabato. Alisubiria kwa sababu ile ile aliyosherehekea ukombozi wa watu wake kutoka Misri siku ya Sabato. Yesu alipumzika siku ya Sabato ikiwa ni kusherehekea kile alichokitimiza!)

III. Sabato na Kanisa la Awali

A. Padre wa kanisa la awali, Ignatius wa Antiokia, kwenye barua yake kwa “Magnesians 9-10” anasema, “Kama wale waliokuzwa kupitia kwenye mfumo wa kale hivi sasa wana matumaini mapya, hawaitunzi tena Sabato, lakini wanaishi kwa kuishika/kuitunza Siku ya Bwana, ambapo maisha yetu yamechipushwa tena na Yeye na ufufuo Wake….. Ni upuuzi kumkiri Kristo Yesu, na kufanya mambo ya Kiyahudi. Kwa maana Ukristo haukuikumbatia dini ya Kiyahudi, bali dini ya Kiyahudi iliukumbatia Ukristo.”

1. Je, ni sababu ipi/zipi ambazo Ignatius anazitoa za kuabudu siku ya Jumapili? (Ufufuo wa Yesu siku ya Jumapili. Uhasama dhidi ya dini ya Kiyahudi.)

a. Je, Wayahudi walikuwa maarufu kwa kiwango gani kipindi ambacho Rumi iliiharibu Yerusalemu na hekalu mwaka wa 70 BK?

b. Je, dini ya Kiyahudi ina ugomvi na Ukristo? (Hii inatupatia mtazamo wa wazi kabisa wa sababu za kuitunza siku ya Jumapili hapo awali. Imejengwa kwenye hoja ya “kimantiki” ambayo sio bora zaidi kuliko mantiki ya Yesu kupumzika siku ya Sabato baada ya kuteswa kwake. Kwa kuongezea, ina upande wa pili wa chuki kubwa ya Wayahudi. Ilikuwa ni baada ya kujiingiza kwenye mjadala wa dhati wa kiteolojia na mmojawapo wa mafariki wangu wa Kiyahudi ndipo nilipoelimishwa kuhusu uhusiano wa karibu wa historia kati ya uhasama/chuki/uadui dhidi ya Wayahudi na ukataaji wa Sabato ya Kibiblia. Uhasama dhidi ya Wayahudi (mfikirie Musa, Petro, Paulo) hauna msingi wa kiteolojia, na hauna nafasi sahihi kwenye fikra zetu. Yesu alikuja kutimiliza, sio kutangua, unabii na matendo ya Agano la Kale. (Mathayo 5:17.)

B. Mfalme Konstatino wa Rumi katika mwaka wa 321 BK alitangaza rasmi Jumapili kuwa siku mpya ya mapumziko kwenye himaya yake. Hivi sasa ninasoma kitabu maarufu sana kuhusu historia ya Yerusalemu. Kinasema kuwa Konstatino alikuwa na matamanio mawili makubwa, uwezo/nguvu ya jua na Ukristo. Alitengeneza sarafu zenye sanamu ya msalaba na nyingine zenye sanamuya jua. Je, hii inapendekeza nini kwenye mtazamo wake wa ibada ya Jumapili? (Alitaka Wakristo wajumuishe ibada ya jua kwenye ibada zao za kidini.)


1. Baadhi ya Wakristo wanasema kuwa hawaijali Krismasi au Pasaka kwa sababu zina mizizi ya “kipagani.” Ninakataa hoja hizi kwa sababu ya umuhimu wa hizi sherehe za kidini kwa Wakristo hivi leo. Je, tunapaswa pia kuwa na mtazamo huo huo kuhusiana na ibada ya kila juma wa Sabato ya Jumapili? (Huo ungekuwa mtazamo wangu kama isingekuwa ni kwa ajili ya amri ya Biblia iliyo wazi kabisa na isiyoyumba kwamba siku ya saba ndio pekee iliyofanywa na Mungu kuwa takatifu. Krismasi na Pasaka kamwe hazikudhihirishwa kuwa takatifu katika Biblia, kwa hiyo nipo huru kudai umuhimu wao wa sasa kwa Wakristo wote waliopo duniani.)

IV. Siku Yetu ya Bwana

A. Jina la kawaida la Jumapili ni kuiita kuwa siku ya Bwana. Je, Yesu aliabudu siku ya Jumapili au alitoa ishara yoyote kuwa aliikana/aliikataa Sabato? Hebu tusome Mathayo 12:1-2. Kama Yesu alitaka kutoa ishara ya kubadili ibada kutoka Sabato kwenda kwenye siku nyingine, je, hii ingekuwa fursa nzuri sana kufanya hivyo?

B. Soma Mathayo 12:3-5. Je, kuna wazo gani lililopo kuhusu utakatifu wa Sabato kwenye haya mafungu? (Analinganisha kula mikate ya wonyesho na wanafunzi wake kula siku ya Sabato – hakuna hata kimojawapo kilicho halali. Analinganisha makuhani kufanya kazi siku ya Sabato na wanafunzi wake “kufanya kazi” siku ya Sabato. Anasema kuwa “hawana hatia,” lakini sio kwa sababu ya tatizo lolote lililopo dhidi ya Sabato.)

C. Soma Mathayo 12:6-8. Kwa nini Daudi hakuwa na hatia, makuhani hekaluni hawakuwa na hatia, na wanafunzi wa Yesu hawakuwa na hatia kwa kuivunja Sabato? (Lengo kuu. Daudi kwa dhati kabisa alikuwa na haki ya kufanya hivi kwa kuwa alikuwa mtiwa mafuta wa Mungu. Makuhani walikuwa wakifanya kazi kwa ajili ya Mungu. Yesu alikuwa Mungu na wanafunzi wake walikuwa pamoja naye katika kuuendeleza Ufalme wa Mungu.)

1. Je, Yesu anamaanisha nini anaposema, “Nataka rehema, wala si sadaka?” (Soma Hosea 6:6. Dhana ya kutembea kwetu na Mungu sio kutoa wanyama sadaka (kutubu dhambi), ni kumpenda na kumtii Mungu. Washtaki wa wanafunzi walikuwa mbele za Mungu, lakini macho yao bado yalikuwa kwenye jambo dogo (lisilo la msingi). Yesu alikuwa hashushi umuhimu wa Sabato. Alikuwa akiwaelekeza wafuasi wake kujikita kwenye jambo la muhimu katika suala lolote lile.)

a. Je, watunzaji wa Sabato watalitumiaje somo hili hivi leo?

D. Soma Yohana 9:10-11 na Yohana 9:13-16. (Niliwahi kuwa na mshiriki wa darasa ambaye alimshutumu kwa nguvu zote Billy Graham kwa kutoitunza Sabato. Haya ndio mashtaka yaliyofanywa na baadhi ya Mafarisayo.)

E. Soma Yohana 9:35-41. Je, Yesu anamaanisha nini anaposema kuwa amekuja ili vipofu wapate kuona? (Kwa mara nyingine tena Yesu anazungumzia kuhusu kuwa na mtazamo sahihi juu ya Sabato na asili ya umuhimu wake. Graham aliwaongoa mamia kwa maelfu ya watu maishani mwake. Huenda zaidi ya mtu mwingine yeyote yule, alikuwa uso (kioo) cha Wakristo wa Kiprotestati kwa miongo kadhaa. Mshiriki mwenzangu wa darasa, ambaye huenda kamwe hajawahi kumwongoa mtu yeyote, hakujikita kwenye Ufalme wa Mungu. Yesu anatuita tujikite kuuendeleza Ufalme wa Mungu.)

F. Soma Mathayo 12:9-12. Je, Yesu anaukataa utakatifu wa Sabato? (Hapana.)


1. Je, Yesu anasema nini kuhusiana na Sabato? (Kwa mara nyingine, anasema kuwa tunatakiwa kuiangalia vizuri - zana ya kuuendeleza Ufalme wa Mungu. Kuwaponya na kuwasaidia watu wengine kunaendana na Sabato.)

G. Soma Mathayo 12:13-14. Je, ingejalisha kitu chochote kwa yule mtu kama Yesu angesubiria hadi muda wa jua kuzama ili aweze kumponya? (Hapana.)

1. Je, kwa nini Yesu alimponya siku ya Sabato? (Kusisitiza dhana yake ya jinsi ambavyo Sabato inapaswa kueleweka.)

2. Kama Yesu alikuwa anakaribia kuifuta Sabato, kwa nini alifanya juhudi hizi za kubainisha jinsi Sabato inavyoingia kwenye mpambano kwa ajili ya Ufalme wa Mungu?

H. Rafiki, Sabato ni ukumbusho wa kile ambacho Yesu amekifanya kwa ajili yetu – Alituumba, alituokoa kutoka dhambini, alikufa kwa ajili yetu na alifufuka kwa ajili yetu. Kamwe hatutakiwi kuacha kusherehekea siku takatifu aliyotupatia na kamwe haijabadilika. Lakini, lazima pia tuwe na mtazamo sahihi juu ya Sabato katika kuuendeleza Ufalme wa Mungu. Je, utakubali hivi leo kuitunza Sabato kama sehemu ya kazi yako ya kuuendeleza ufalme wa Mungu?

V. Juma lijalo: Utunzaji wa Viumbe

Wednesday, February 8, 2012

Somo la 6: Mungu Mtoaji wa Sheria

Somo limetafsiriwa na Mgune Masatu

(Kutok 19 & 20, Mathayo 22, Isaya 48)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: Somo lililopita tulijifunza kitabu cha Wagalatia, somo ambalo lilitupatia mtazamo wa “sheria dhidi ya neema.” Mtazamo huo utatupotosha isipokuwa tu kama tutafungua macho yetu kwenye mtazamo mpana zaidi. Hebu angalia hapa duniani kwenye nchi zinazoongozwa kwa sheria na uzilinganishe na nchi zinazoongozwa na chochote kile ambacho mtawala anaamua kwa muda huo. Nchi ambazo zinaongozwa kwa “utawala wa sheria” zina mafanikio zaidi na zina uhuru zaidi. Uhuru wa kidini, uhuru wetu wa msingi sana, unapatikana tu kwenye nchi zinazoongozwa chini ya utawala wa sheria. Kama wazo lako la “neema” lina dhana ya kwamba unafanya jambo lolote unalodhani kuwa ni zuri kulifanya kwa wakati huo, basi hapo utakuwa umekosea kabisa dhana ya sheria ya Mungu. Hebu tuzame kwenye somo letu la Biblia ili tuweze kujifunza zaidi kuhusu sheria ya Mungu.

I. Utoaji (“Ofa”)

A. Soma Kutoka 19:3-6. Je, Mungu anatoa ofa ya kitu gani? (Anatoa ofa ya mkataba. Yaani kama watu “watatunza agano langu” watakuwa watu maalum kwa Mungu.)

1. Unadhani Mungu alikuwa anamaanisha nini aliposema kuwa watu watakuwa “ufalme wa makuhani?” (Je, makuhani wanafanya nini? Wao ni wawakilishi wa mungu wao. Mungu anatupatia mahusiano maalum endapo tutamtii.)

2. Kwa nini watu watake kukubali ofa hii? (Kama Mungu alivyokwishawaelezea, alikuwa na uwezo mkubwa kabisa wa kushughulikia matatizo yote waliyokabiliana nayo.)

B. Soma Kutoka 19:7-8. Je, watu waliikubali ofa ya Mungu?

II. Muhtasari

A. Soma Mathayo 22:37- 40. Yesu aliposema kuwa “Torati na Manabii” “inaning’inia” kwenye hizi amri mbili, je, alimaanisha nini? (Hizo ndizo msingi na umuhimu wa sheria.)

1. Angalia wajibu wetu kwa Mungu. Je, ni sehemu yetu gani ambayo Mungu anaitaka? (Yote.)

2. Yesu anaporejea “moyo,” “roho” na “akili,” je, unadhani kuwa anamaanisha nini? Je, hivi vitu vitatu ni tofauti?

3. Je, ni kwa jinsi gani amri ya pili (mpende jirani yako) ina utofauti kwa muktadha wa kujitoa kwayo na ile ya kwanza (mpende Mungu wako)? (Hatuambiwi kuwapenda majirani zetu kikamilifu kabisa, bali tuwapende kama tunavyojipenda wenyewe.)

a. Je, unajipenda kwa kiwango gani?

b. Je, ni sahihi kujipenda wewe mwenyewe? (Ama kwa hakika kabisa!)


B. Je, unadhani kuwa Yesu anaanzisha njia mpya ya kuiangalia sheria? (Soma Kumbukumbu la Torati 10:12. Yesu haanzishi kitu kipya.)

III. Amri Kumi za Mungu - Upendo kwa Mungu

A. Soma Kutoka 19:16-19. Utabaini kuwa hii ni tofauti na njia ambayo Yesu aliutangaza msingi wa sheria kwenye Mathayo 22. Kwa nini Mungu aliwatisha watu? (Alitaka kusisitizia umuhimu wa sheria. Pia alitaka (ukisoma mafungu yanayofuatia) kuwaweka watu mbali ili kwamba wasijaribu kumwona na wafe.)

B. Soma Kutoka 20:1-2. Je, Mungu angeongezea kitu gani kwenye wasifu wake hivi leo? (Mimi ni Bwana Mungu wako niliyekuokoa kutoka katika mauti ya milele.)

1. Je, haya ni madai makubwa zaidi kuliko yale ya awali?

C. Soma Kutoka 20:3. Je, hii inapendekeza nini kuhusiana na Mtoaji wetu wa sheria? (Kwamba anahitaji utii wetu uwe wa kwanza kabisa.)

D. Soma Kutoka 20:4-6. Ni kwa nini hii amri ya pili ni ya muhimu ukizingatia kuwa tayari tunayo ile amri ya kwanza? (Hii inahusiana na heshima/hadhi/utu wa Mungu. Mungu hataki kushushwa na kuonekana kuwa kama “kitu fulani hivi” – hususan, sio kuwa kama kitu alichokiumba, au kitu kilichofanywa/kilichotengenezwa na kimojawapo cha uumbaji wake.)

1. Je, ninapindisha maneno ya Mungu? Anasema kuwa ana “wivu” na nilipendekeza kuwa hiyo ndio ilikuwa hadhi yake. Je, vitu hivi viwili vinatofautiana? (Yesu anaionea wivu nafasi yake – hadhi yake.)

2. Nini kinatokea kwa kumpa Mungu kile anachokistahili? (Mibaraka! Mibaraka hadi kwa watoto wetu.)

E. Je, unawezaje kuzielezea kwa ufupi hizi amri mbili za kwanza? (Zinaakisi somo letu la juma lililopita – zinaonyesha kuwa Mungu ni mtakatifu, amewekwa wakfu, na ni wa kipekee.)

F. Soma Kutoka 20:7. Je, ni kitu gani cha kwanza kabisa kinakujia akilini unapoisoma amri hii? (Kuapa.)

1. Je, unadhani kuwa ni tatizo gani lililopo ambalo Mungu analielezea? Je, ni kwa jinsi gani kuapa ni tatizo kubwa kwenye hilo tatizo lililoelezewa? (Kwa mara nyingine tena, ni utu/hadhi, utukufu wa Mungu, ndilo lililo suala la msingi.)

2. Je, utakuwa unakiuka amri hii kwa wewe kudai kuwa Mkristo na kufanya mambo ambayo yatampa Mungu sifa mbaya? (Nadhani hili ni tatizo kubwa zaidi kuliko kuapa. Watu wanafikiria kwa uchache kuhusiana na kuapa, kwa sababu kwa ujumla wale wanaoapa sio watu wanaodai kuwa wawakilishi wa Mungu. Ni wale wanaodai kuwa wawakilishi, na wale wanaofanya uovu, ndio wanaolitumia vibaya jina lake.)

IV. Amri Kumi – Kipindi cha Mpito

A. Soma Kutoka 20:8-11. Je, hii amri ya nne inahusu kumpenda Mungu au inahusu kuwapenda wanadamu wenzetu? (Inamheshimu Mungu kwa kuwa Muumba wetu, lakini wanadamu wote (hadi waajiriwa wetu) wanafurahia pumziko hili la kila juma.)

V. Amri Kumi - Upendo kwa Jirani


A. Soma Kutoka 20:12. Je, kwa nini heshima kwa wazazi wetu inahusishwa na urefu wa maisha yetu? Je, Mungu anatuambia kuwa “atatushambulia/atatupiga” kwa kutowaheshimu wazazi? (Kwa ujumla wazazi wana busara. Kama tukijifunza kutoka kwao maisha yetu yatakuwa bora na marefu. Kuwapenda wazazi wetu, kama kuwapenda wenzi wetu, ndio njia ya kujipenda sisi wenyewe.)

B. Soma Kutoka 20:13-16. Je, ni kitu gani kinachofanana kinachoonekana kwenye hizi amri zote? (Soma Warumi 13:8-10. Upendo wa watu wengine. Tunapotoa/tunapochukua kutoka kwa watu kitu chao cha haki, tunaonyesha ubinafsi na upungufu wa upendo.)

1. Je, ni kitu gani alichotutendea Yesu? (Alikufa badala yetu. Aliyatoa maisha yake kwa ajili yetu.)

a. Je, amri hizi zinaakisije kile alichotutendea Yesu? (Msingi wa injili ni kujitoa sisi wenyewe kwa ajili ya watu wengine. Matendo yaliyoelezewa kwenye hizi amri yanachukua vitu kutoka kwa watu wengine kwa faida yetu. Amri hizo ni kinyume cha injili.)

C. Soma Kutoka 20:17. Je, hii inahusianaje na amri nne ambazo tumejifunza hivi punde? (Hii ni sehemu ya mtazamo wa amri zilizotangulia. Ukijiepusha kutaka vitu vya jirani yako, kama ukiridhika na kitu chako, basi hutachukua kitu chochote cha jirani yako.)

1. Je, upendo kwa jirani yako unaingiaje kwenye hii amri ya mwisho?

2. Je, hizi kanuni za Kibiblia zinapaswa kujihusisha na sera za kodi za kitaifa?

3. Kama umesema kuwa ndiyo, Marekani inapokuwa inaingia kwenye miezi ya mwisho ya uchaguzi wa urais, kuna mjadala mkubwa kuhusu kuongeza kodi ya ziada kwa matajiri. Je, huu ni ukiukwaji wa amri ya kumi? Je, huu ni wivu na matamanio?

VI. Amri Kumi za Neema

A. Soma Isaya 48:17. Je, haya ni maelezo ya Amri Kumi? (Haya ni sehemu ya maelekezo ya Mungu “ya jinsi ambavyo unapaswa kuenenda.”)

B. Soma Isaya 48:18-19. Je, matokeo ya kuitii sheria ya Mungu ni yapi? (Amani. Haki. Hadhi. Familia. Haya ndio mambo yote tunayoyataka. Mungu anatufundisha kuwa sheria yake haipo kwa ajili ya kutukosesha. Haipo kwa ajili ya kutuhukumu/kutushutumu. Mungu alitupatia sheria yake kwa sababu anatupenda na anafahamu vizuri zaidi kuwa ni mtazamo na matendo ya aina gani yatakuwa mbaraka maishani mwetu.)

VII. Juma lijalo: Bwana wa Sabato

Wednesday, February 1, 2012

Somo la 5: Utakatifu wa Mungu

Somo limetafsiriwa na Mgune Masatu

(1 Petro 1, Mwanzo 2, Ayubu 42, Luka 5)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: Biblia inatuambia kwa kurudia rudia kuwa Mungu ni mtakatifu. Je, hiyo inamaanisha nini? Hili sio suala linalomaanisha kufurahisha akili zetu tu, kwa sababu Mungu anatuamuru kwenye Agano la Kale na Agano Jipya la Biblia kuwa tuwe watakatifu kama jisi Mungu alivyo mtakatifu. (1 Petro 1:15-16; Mambo ya Walawi 11:44.) Kama hatuelewi kile kinachomaanishwa kwa Mungu kuwa mtakatifu, hatuwezi kuelewa lengo la muhimu maishani mwetu. Hetu tuone tunavyoweza kulibaini hili kwa mara nyingine tena kwa kuzama kwenye somo letu la Biblia!

I. Wakati (Muda) Mtakatifu

A. Soma Mwanzo 2:2-3. Hii inatuambia kuwa Mungu “aliifanya” Sabato kuwa takatifu. Je, muktadha huu unapendekeza kuwa utakatifu unamaanisha nini? (Kwanza kabisa, utakatifu unatoka kwa Mungu. Yeye ndiye mwanzilishi wake. Pili, kuwa takatifu ni kuwa tofauti na siku nyinginezo. Utabaini kuwa utakatifu na mibaraka vinaonekana kufanana. Siku takatifu ni siku iliyowekwa wakfu dhidi ya siku nyinginezo, siku maalum, siku iliyobarikiwa.)

B. Soma Zaburi 86:8-10. Je, ni kipengele gani cha utakatifu wa Mungu kinachofanana na Sabato? (Mungu amewekwa wakfu. Hakuna mungu kama Bwana wetu. Yeye peke yake ndiye mkuu na mzuri ajabu.)

C. Soma Kutoka 20:11. Je, uhusiano iliopo kati ya huu muda mtakatifu na Uumbaji ni upi? (Ni sherehe, ukumbusho wa uwezo wa ubunifu wa Mungu.)

1. Kama haya mawazo kuhusu utakatifu wa Mungu pia yanahusika kwetu kwa namna fulani hivi, je, ni sehemu gani ya kitendawili cha utakatifu tunachoweza kukifahamu? (Utakatifu unatoka kwa Mungu pekee. Inamaanisha kuwa tumewekwa wakfu na kubarikiwa pia. Inamaanisha kuwa maisha yetu yanapaswa kuwa kama usherehekeaji wa uwezo wa Mungu na ubunifu wa Mungu.)

D. Soma 1 Samweli 2:2. Tunapozama kwenye mjadala kuhusiana na utakatifu wa Mungu na lengo la utakatifu wetu, je, hii inatufundisha kitu gani cha muhimu? (Hatuwezi kufikia kiwango cha Mungu cha utakatifu. Hakuna hata mtu mmoja aliye kama yeye! Habari njema ni kwamba hatupaswi kukata tamaa pale ambapo utakatifu wetu mara kwa mara unaonekana kuwa kwenye matatizo.)

E. Soma Kutoka 20:8-10. Je, ni kwa namna gani kuacha kufanya kazi kuna cha kujihusianisha na muda mtakatifu? (Ni wakati wa kujielekeza kwenye kile alichokiumba Mungu, sio vile tunavyovifanya. Hii inaonyesha kuwa utakatifu unatoka kwa Mungu, sio kwetu. Hatutengenezi/hatufanyi muda mtakatifu kwa kufanya jambo fulani.)

1. Je, ni kipande gani kingine cha kitendawili kinaimarishwa na suala hili kuhusiana na sisi kuwa watakatifu? (Hatuwezi kujifanya wenyewe kuwa watakatifu.)

II. Akili Takatifu


A. Soma 1 Petro 1:13-16. Je, tumefanya makosa? Petro anatuambia tuwe watakatifu katika yote tuyatendayo. Je, hiyo inamaanisha kuwa tunaweza kuufanya/ku-uumba utakatifu?

1. Angalia tena 1 Petro 1:13. Je, ni “tendo” gani linafanyika hapa? (Hakuna tendo lolote. Petro anatuambia tu kuwa tujielekeze kwenye zawadi ya neema ya Mungu. Zingatia/kuwa msikivu. Neema (utakatifu?) tunayoipokea “tunapewa,” hatuipati kwa juhudi zetu.)

2. Vipi kuhusu 1 Petro 1:14, ambapo tunaambiwa kuwa “watiifu?” (Tunapojielekeza kwa Bwana wetu, tunajifunza zaidi kuhusiana na mapenzi yake. Kimsingi Petro anasema, “Mmejifunza, kwa hiyo msiishi kufuatana na matamanio yenu maovu.”)

B. Soma 1 Petro 1:17-19. Je, matendo ni sehemu ya kuishi maisha matakaifu? (Ndiyo. Wakati ambapo hatuwezi kujifanya wenyewe kuwa watakatifu, Mungu anatutaraji tuishi maisha yanayoendana na kuwa watakatifu. Lengo la kwanza ni kuzingatia mapenzi ya Mungu. “Je, ninaweza kufanya jambo gani hivi leo ili kuuendeleza Ufalme wa Mungu, badala ya kukiendeleza chanzo cha dhambi?”)

1. Je, kuishi kama “wageni” na “kwa hofu yenye utii” kuna nini cha kujihusisha na lengo letu la utakatifu? (Hatutakiwi kuridhika sana na maisha ya hapa. Sisi sio sehemu ya hii dunia. Sisi ni sehemu ya Ufalme wa Mungu. Kwa hiyo, “tunamhofu” (ikimaabisha heshima, inayohusiana na Mungu). Hatujihusishi na dunia ila kuuendeleza Ufalme wa Mungu.)

2. Je, ni tofauti gani iliyopo ya kwamba tunafidiwa na kafara ya Yesu mwenyewe, badala ya malipo ya fedha? (Inafanya jinsi tunavyoishi maisha yetu yawe ya mtu binafsi. Yesu alilipa gharama kwa ajili ya dhambi zetu kwa kuyatoa maisha yake. Haliwezi kuwa suala la binafsi zaidi ya hapo. Tunahitajika kulichukua lengo la utakatifu na kulifanya kuwa suala la mtu binafsi.)

C. Soma 1 Petro 1:20-21. Je, ni hoja gani unayoiona hapa kuhusiana na neema? (“Tunaamini katika Mungu” kupitia “kwake” – kupitia kwa kile Yesu alichotutendea pale msalabani na katika ufufuo wake.)

D. Soma 1 Petro 1:22. Kwa wazi kabisa hii inaonyesha kuwa kile ambacho nimekuwa nikikifundisha ni makosa, sawa? Kinasema kwamba “tumejitakasa roho zetu kwa kuitii kweli.” Je, ni nini kinachoweza kuwa wazi zaidi ya hicho?

1. Angalia sehemu iliyosalia ya hili fungu. Je, unaweza kusaga meno yako na kumpenda mtu ambaye unamwona kabisa kuwa hapendeki? Vipi kuhusu “upendo wa dhati” kutoka moyoni? (Sote tunafahamu kuwa upendo wa dhati wa “ndugu” unatoka tu kwenye moyo uliobadilishwa na Mungu. Moyo unaotambua kuwa Mungu alikufa kifo cha kutisha kwa ajili yetu, ni moyo unaojibu kwa shukrani na upendo. Upendo wa ndugu ni mwitikio kwa Mungu. Kwa hiyo Mungu, na sio mapenzi ya mwanadamu, ndicho chanzo cha upendo. Hata hivyo, ni kweli kwamba “tabia” ya utii (kinyume na “tabia” ya kutokutii) inasaidia katika njia ya kuuelekea utukufu.)

III. Utukufu Linganishi


A. Sehemu kubwa ya kitabu cha Ayubu kinajumuisha maneno ya Ayubu akijitangazia kutokua na hatia ilhali marafiki zake wanasisitiza kuwa anaadhibiwa kutokana na dhambi zake. Suala la kuvutia linakuja pale ambapo Ayubu anatangaza kuwa anataka awe na Mungu chumbani na amfanye ajibu baadhi ya maswali yake kuhusu usawa na haki. Katika kitabu cha Ayubu sura za 40 & 41 Mungu anamtokea Ayubu na anamwambia kuwa watakuwa na “uendeshaji wa mashtaka,” lakini hali itakuwa ni kwamba Ayubu ndiye atakayekuwa akijibu maswali. Hebu tusome Ayubu 42:1-3. Je, jibu la awali la Ayubu kwa Mungu ni lipi? (Nilijibu nikiwa mpumbavu. Sikuelewa uwezo na utukufu wa Mungu.)

B. Soma Ayubu 42:4-6. Je, utukufu na utakatifu wa Mungu vinatenda kitu gani kwa Ayubu? (Kutubu kwa unyenyekevu. Uelewa wa kwamba hatupo kwenye nafasi ya kuhoji haki na asili ya Mungu.)

1. Je, hii inakubalianaje na mjadala wetu wa awali kuhusiana na kile kinachomaanishwa kwa kuwa mtakatifu? (Kuwa mtakatifu ni “kuwekwa wakfu.” Mungu “amewekwa wakfu” kutoka kwetu. Kamwe hatuwezi kuwa na tumaini la kuweza kuufikia utakatifu wa Mungu. Tunapokea zawadi ya utakatifu anayotupatia na kudhamiria kutembea kwenye njia inayotuelekeza kwenye utakatifu. Kutembea katika njia hiyo hakutegemeani na suala la kama tunaelewa matatizo yote maishani. Kile tunachokielewa ni kwamba Mungu wetu ni mkuu, mwenye upendo na mtakatifu.)

C. Soma Luka 5:1-5. Hebu jiweke kwenye nafasi ya Petro. Je, mawazo yako kuhusu amri ya Yesu ni yapi? (Walikuwa wamekwisha safisha zana zao na vifaa vyao. Yesu anawataka wachafue zana zao ili kwamba waje waifanye kazi hiyo tena. Wanavua samaki usiku, na walikuwa wametia juhudi kubwa sana usiku kucha. Yesu anawaambia kufanya kazi ya ziada. Wao ni wataalam wa uvuvi, Yesu ni mhubiri. Wao wana maarifa makubwa kuhusiana na suala hili.)

D. Soma Luka 5:6-8. Kwa nini hii inaonyesha kuwa Petro ni mdhambi? Alimtii Yesu? (Petro anatambua kuwa yeye sio mwerevu ambaye anajiendekeza kwa Yesu tu. Anatambua kuwa yupo mbele ya nguvu ya ulimwengu. Kitu kitakatifu kimekutana na kisicho kitakatifu na kitiifu, na utakatifu unahitaji utenganifu!)

E. Soma Luka 5:10 (sehemu ya mwisho). Je, kwa nini Yesu asiogope? (Kwa sababu yupo kwenye utume wake kuwapatanisha Mungu Mtakatifu na wanadamu wadhambi. Safari yetu ya kuuelekea utakatifu ni ya “kuwavua watu,” kuuendeleza Ufalme wa Mungu.)

F. Rafiki, je, utaufanya utakatifu kuwa lengo lako hivi leo? Je, malengo, maazimio, matamanio na matendo yako, yatajielekeza katika kuuendeleza Ufalme wa Mungu? Je, utafanya uchaguzi huo sasa hivi?

IV. Juma lijalo: Mungu Mtoaji wa Sheria.

Tuesday, January 24, 2012

Somo la 4: Mungu wa Neema na Hukumu

Somo limetafsiriwa na Mgune Masatu

(Yohana 3, Hesabu 21, Ufunuo 14)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: Juma hili tunajifunza vipengele viwili vya Mungu: neema na hukumu. Ukisoma mafungu machache yanayohusu hukumu – hususan ukirejea hukumu inayolenga matendo – unaweza kushangaa jinsi ambavyo neema na hukumu vinavyoendana sawia kwenye injili hiyo hiyo. Kimsingi, kwa muda mrefu sana nimekuwa nikiichukulia kwa dhati sana dhana ya kwamba Yesu mara kwa mara huwa anarejea hukumu inayotegemea matendo ilhali Paulo ana kaulimbiu madhubuti ya wokovu kwa njia ya neema. Je, tunaweza kuhusianisha hayo mawazo mawili pamoja? Kama hivyo ndivyo, je, ni kwa manma gani tutafanya hivyo? Hebu tuzame kwenye somo letu la Biblia ili tuweze kuona kile tunachoweza kujifunza!

I. Hukumu

A. Soma Mathayo 12:36-37 na Mathayo 16:27. Je, Bwana wetu anasema kuwa kiwango cha hukumu ni kipi? (Maneno yetu na matendo yetu!)

B. Soma 2 Wakorintho 5:10. Aaaah la! Huyu ni Paulo. Je, Paulo anasema kuwa msingi wa hukumu ni upi? (Matendo yatendwayo “katika mwili.”)

C. Je, kitu gani kinaendelea hapa? Ni majuma machache tu yaliyopita tulijifunza kwenye kitabu cha Wagalatia kuwa tunaokolewa kwa neema. Hebu tulichukulie suala hili katika hali ya mtu binafsi kuhusu hukumu inayotokana na matendo. Je, unataka watu wengine wasimamishwe na kuandikiwa kulipa faini kwa kuendesha kwa mwendo wa kasi barabarani? (Ndiyo! Hususan pale wanapoendesha kwa mwendo wa kasi kwenye maeneo yetu tunapoishi.)

1. Vipi kuhusu wewe – je, unataka polisi akuandikie kulipa faini kwa kuendesha kwa mwendo wa kasi? (Hii inathibitisha taswira pana zaidi, tunataka hukumu kutegemeana na matendo ya watu wengine, sio kwa ajili yetu wenyewe.)

2. Je, tunadhani kuwa watu wengine wanastahili hukumu kutokana na matendo yao, lakini sisi (walao mimi) tuwe na uwezo wa kuepuka hukumu? (Tunaweza kuona kwamba somo hili ni gumu kidogo kwa sababu tuna upendeleo wa asili dhidi ya hukumu zetu. Hatutaki kupata kile tunachostahili, lakini tungependa watu wengine wakipate kitu hicho hicho.)

II. Nyoka Jangwani

A. Hebu tuone kama tunaweza kulichukulia suala hili ukiachilia mbali upendeleo wetu. Soma Yohana 3:14-18. Je, Yesu anajichanganya? Yesu anawezaje kusema hapa kuwa imani katika yeye ndio msingi wa uzima wa milele, lakini hapo awali alisema kuwa matendo ndio yalikuwa msingi wa hukumu? (Utabaini kuwa Yesu alikuwa anarejea mtu “anayeshutumiwa” badala ya kuhukumiwa.)


1. Juma lililopita tulijadili huduma ya patakatifu. Mdhambi alipokuja hekaluni na kafara, je, mdhambi alikuwa na hatia? (Ndiyo. Tunahukumiwa kwa matendo yetu – aidha tuna hatia ama hatuna hatia. Na bila kuingia kwa undani zaidi, mara zote huwa tuna hatia kwa sababu ya asili yetu ya dhambi. Mdhambi alipokuja na mwana-kondoo, hakuwa “asiye na hatia,” badala yake hakuhumiwa kwa sababu kafara ililipa adhabu kwa niaba yake.)

B. Je, bado hatuna tatizo na maneno ya Paulo (2 Wakorintho 5:10) kwamba tutahukumiwa kutokana na mambo “mazuri”? Vipi kuhusu Yesu anaposema (Mathayo 5:10) kuwa tutahukumiwa kutokana na mambo “mazuri?” Vipi kuhusu Yesu anaposema (Mathayo 12:37) kuwa maneno yetu yanaweza “kututendea vizuri/vyema?”

C. Hebu tuendelee kusoma katika Yohana 3 ili tuone kama tunaweza kuona kidokezo chochote. Soma Yohana 3:19-21. Sasa tuna kitu kipya, “nuru!” Je, nuru ina nini cha kujihusisha na wokovu wetu? (Tukiupenda mwanga tunaokolewa, tukilipenda giza hatuokolewi.)

1. Tuna mambo mengi sana yasiyo sawia hapa. Tuna matendo, tuna imani na tuna nuru. Je, unaweza kuunganisha haya mambo yasiyo sawia ili kuleta nadharia yenye mantiki? Au, je, mawazo yote haya ni mkanganyiko tu?

D. Hebu turejee kwenye kisa cha awali (cha asili). Soma Hesabu 21:6-9. Nini kilichosababisha watu wafe? (Nyoka. Hata hivyo, ukiangalia muktadha huo, nyoka walipelekwa pale kama hukumu kwa ajili ya dhambi.)

1. Je, kwa nini Mungu alimwambia Musa awaambie watizame kiwakilishi cha kile kilichowafanya wafe? (Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikifikiria kwamba hiki kisa cha kutisha kinatufundisha kuwa lazima tuziangalie (tuzichukulie kwa dhati, tuzitubu, nk.) dhambi zetu. Hatua ya kwanza ya kuuelekea wokovu ni kuziangalia na kutubu dhambi zetu, na matendo yetu mabaya.)

E. Hebu tusome tena Yohana 3:14-15 na Yohana 3:19-20. Je, ni kwa jinsi gani kisa cha nyoka na kuipenda/kuichukia nuru sasa kinalenta mantiki? (Kwamba kama tukiipenda sana dhambi yetu sana kiasi cha kushindwa kuja nuruni, basi sisi tu kama wale waliokataa kuitazama nyoka. Yesu alileta nuru ya injili. Kuikubali nuru ya injili kimsingi hakuendani na kujificha (kusalia) dhambini. Aidha tutachagua kuzikabili dhambi zetu na kuokolewa kwa neema, au tutapendelea kusalia dhambini na kumkataa Yesu.)

1. Je, mazungumzo yote haya kuhusiana na “matendo” na hukumu sasa yanaleta mantiki? (Kwa mtazamo mwingine, wokovu unahusika sana na matendo yetu. Tukiamua kusalia dhambini, hatutaitafuta neema. Lakini, tukizikabili dhambi zetu na kuzitambua, basi tunao uchaguzi mmoja tu – neema!)

2. Jielekeze zaidi kwenye Yohana 3:21. Je, hii inamaanisha nini: “kile alichokitenda kimetendwa katika Mungu?” (Neema ni kazi ya Mungu. Kama tulivyojifunza kwenye somo letu la Wagalatia, hatuwezi kujipatia wokovu, Yesu tayari amekwishafanya hivyo kwa ajili yetu. Lakini, tunachagua kama “tutaiangalia nyoka,” kama “tutakuja nuruni,” kama tutatubu dhambi zetu na kuepuka hukumu kwa damu ya Mwana-kondoo.)

III. Mfano wa Nuhu

A. Hebu angalia mfano wa jambo hili. Soma Mwanzo 6:5-7. Je, Mungu anafikiri kuwa suluhisho la huu uovu wote ni lipi? (Hukumu!)


B. Soma Mwanzo 6:13, Mwanzo 7:6-10, na 2 Petro 2:5. Je, ilikuwa ni vigumu kiasi gani kwa waovu kuingia kwenye safina? (Walionywa. 2 Petro 2:5 inapendekeza kuwa Nuhu aliwahubiria. Wakati ambapo Nuhu alikuwa akiendelea na juhudi za kujenga safina, mtu mwingine yeyote angeweza kuendelea pia. Waovu walipendelea maisha yao ya sasa (giza), na hawakutaka kuungana na Nuhu (kuja nuruni.))

IV. Hukumu ya Siku ya Mwisho

A. Soma Ufunuo 14:6-7. Je, ujumbe kwa wale wanaoishi katika siku za mwisho ni upi? (Kwamba hukumu ya Mungi i juu yao.)

1. Je, mkabiliono wetu sahihi tunapoikaribia hukumu ni upi? (Utabaini kuwa, haisemi kuwa, “usiache kutenda dhambi,” inasema kuwa kwenye mahusiano sahihi na Mungu. Tunahitajika kumtii (kumcha) Mungu, tunahitajika kumpatia utukufu, na tunahitajika kukiri uwezo wake kama Muumba wa vyote.)

B. Soma Ufunuo 14:8. Je, ni ukweli gani wa muhimu kuhusu hukumu tunaohitajika kuujua? (Kwamba Mungu ameushinda uovu. Wale wasio waaminifu kwa Mungu wanaelekea chini kabisa kwenye kushindwa.)

C. Soma Ufunuo 14:9-11. Je, fungu linasema kuwa wale wanaojihusisha kwenye matendo maovu watahimili nguvu ya hasira ya Mungu? (Hapana. Linasema kuwa wale wanaokataa kumwabudu Mungu, na kumwabudu adui wa Mungu watateseka na hukumu. Kiwango cha hukumu ni utii. Wale wanaokuja nuruni dhidi ya wale wanaosalia gizani.)

D. Soma Ufunuo 14:12. Kwa mujibu wa hii hukumu inayokaribia, je, tunaitwa kufanya kitu gani? (“Malaika” wanaelezewa kuwa kama wale “wanaosalia kuwa waaminifu kwa Yesu.” Imani katika Yesu ni haki kwa imani!)

1. Vipi kuhusu sehemu ya “kutii amri za Mungu?” (Hii inaelezea mjadala wetu wa awali. Tukiyapenda matendo yetu maovu, tutakaa gizani na hatutakuja kwenye nuru ya neema ya Yesu. Lakini, tukiipenda nuru, basi tutataka kuyafanya mapenzi ya Yesu. Tutataka kumtii.)

E. Tafakari mafungu katika Ufunuo 14 ambayo tumeyasoma hivi punde. Je, tofauti ya msingi kati ya wenye haki na wasio na haki? (Wenye haki wanamwabudu na kumtukuza Mungu Muumba wao. Waovu wanaawabudu na kuwatii waovu. Hiki ndicho kinachomaanishwa kwa chapa katika kipaji cha uso (akili) na mkono (matendo). Utajwaji wa kuabudu, uumbaji na amri unapendekeza umuhimu mkubwa wa Sabato ya kila juma, kwani ni muda wa kuabudu, muda wa kumpa Mungu utukufu, na muda wa kusherehekea Uumbaji (“Ikumbuke siku ya Sabato …. maana kwa siku sita [Mungu aliumba].”))

F. Rafiki, hukumu inakuja. Hukumu itategemeana na matendo yetu. Kwa kiwango hicho, hakuna hata mmoja wetu anayeweza kuepuka hukumu. Hata hivyo, Yesu anatupatia njia ya kuepuka ya kuhukumiwa kutokana na matendo yetu maovu. Yeye ni Mwana-kondoo wa Mungu aliyekufa kwa ajili ya dhambi zetu. Tukizikabili dhambi zetu kwa kuzikiri na kuzitubu, basi atazifunika dhambi zetu kwa damu yake. Je, hii ni ofa unayoweza kuikataa? Kama sivyo, kwa nini usiikubali hii leo? Kabiliana na nyoka wa maisha yako ya kidhambi, na utoke kwenye giza na uingie nuruni!


V. Juma lijalo: Utakatifu wa Mungu.

Friday, January 13, 2012

Somo la 3: Mungu Kama Mkombozi

Somo limetafsiriwa na Mgune Masatu

(Mwanzo 3, Mambo ya Walawi 5, Warumi 1 & 5)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: Chukulia kwamba wewe ni kibaka. Unafurahia kuwapiga watu vichwani mwao, na unafaidika kwa kuwaibia fedha. Fikiria tena mbadala ufuatao. Wa kwanza, kama polisi wakikukamata, basi watakutaka uombe msamaha kisha watakuachia. Wa pili ni kwamba, una mjomba tajiri sana ambaye pale unapokuwa umekamatwa anarekebisha mambo kwa gharama zake mwenyewe. Je, utaichukuliaje tabia yako ya kuwa kibaka? Hutalichukulia tatizo lako kwa dhati, si ndio? Hatuhitajiki kufikiria kwamba sisi ni vibaka, kwani kiukweli sisi sote ni vibaka kwa namna fulani. Dhambi zetu zinawagharimu watu wengine na kuwagharimu fedha. Hebu tuzame kwenye somo letu la Biblia na kulitafakari tatizo letu na hitaji la Mkombozi!

I. “Ukibaka”/Ukabaji wa Kwanza

A. Katika kitabu cha Mwanzo sura ya 3 tunasoma kisa kinachoelezea jinsi ambavyo Adamu na Hawa walivyotenda dhambi. Hebu tukiangalie kisa hicho kwa kusoma Mwanzo 3:9-13. Je, ni mtazamo wa aina gani walio nao Adamu na Hawa kuhusu dhambi yao? (Wanalaumu wengine.)

B. Soma Mwanzo 3:14-15. Je, Mungu anamaanisha nini anapomwambia nyoka kuwa kichwa chake kitapondwa? (Mungu haongei na nyoka tu, anaongea na Shetani. Anamwambia Shetani kwamba atashindwa.)

1. Je, ushindi wa Mungu na kushindwa kwa Shetani vinahusisha kitu gani? (Ni punde tu Shetani alikuwa ameupata utii wa wanadamu. Ni punde tu alikuwa ameingiza dhambi duniani. Dhambi itapaswa kushindwa na utii wa wanadamu kurejeshwa.)

II. Upatanisho kwa Vibaka

A. Soma Mambo ya Walawi 5:5-6. Je, Mungu alitumia njia gani katika kukabiliana na tatizo la dhambi? (Kwamba dhambi lazima iungamwe, na mnyama achinjwe “ili kufanya upatanisho kwa ajili ya dhambi.”)

B. Soma Mambo ya Walawi 17:11. Je, unaweza kuelezea mantiki ya mfumo wa kafara? (Dhambi inamwelekeza mtu mautini. Matokeo na adhabu ya dhambi ni kifo. Mungu aliweka mpango ambao maisha ya kitu kingine yangeweza kulipa adhabu kwa ajili ya dhambi zetu.)

C. Soma Yohana 1:29. Je, Yohana Mbatizaji alisema nini kumhusu Yesu? (Kwamba alikuwa “Mwana-kondoo wa Mungu” ambaye “ataichukua dhambi ya ulimwengu!”)

1. Kama ungekuwa umekaa mahali pale ukimsikiliza Yohana, je, ungehitimisha nini kuhusu mfumo wa kafara na Yesu? (Kwamba mfumo wa kafara ulikuwa unajielekeza kwa Yesu. Ulikuwa ni aina ya unabii. Kwamba kama vile kondoo alivyomwaga damu yake ili kupatanisha dhambi, ndivyo ambavyo Yesu atamwaga damu yake ili apatanishe dhambi zetu.)


III. Matokeo ya Kubaka

A. Soma Luka 1:26-32. Linganisha jinsi ilivyokuwa kwa Yesu kule mbinguni na jinsi alivyokuwa alipokuja kuishi duniani kama mwana wa Mariamu?

1. Hebu niambie yale yote aliyoyaacha Yesu?

B. Soma Mathayo 27:27-31, Matendo 2:23-24, na Mathayo 27:39-42. Je, Yesu aliacha vitu gani?

C. Soma Warumi 5:6-8. Je, Yesu alikuwa akifanya kitu gani alipokufa pale msalabani (kitu cha aibu sana kwa Mungu)? (Alikufa kwa ajili ya dhambi zetu.)

1. Je, ungefanya kile alichokifanya Yesu kama ungekuwa yeye?

2. Je, mtazamo wa Yesu ulikuwa upi? (Haukuwa kwamba tungeweza kufanya kitu chochote kwa ajili yake. Hatukuwa na “uwezo wowote.” Haikuwa kwamba tulikuwa na ustahili wowote. Tulikuwa “wadhambi.” Ilikuwa ni kwa sababu ya upendo tu.)

D. Soma Warumi 5:9. Je, Mungu anawezaje kutughadhibikia na wakati huo huo kutupenda? (Hasira ya Mungu i dhidi ya dhambi zetu.)

1. Kwenye mfululizo wetu wa masomo uliopita, nilipendekeza kwamba tunapaswa kuonyesha matendo yetu kwa kusema kuwa, “Je, hii itampendeza Mungu? Je, hii itamfurahisha mwenza wangu?” Je, ghadhabu ya Mungu inaingilianaje na hili suala?

2. Je, inaleta mantiki kwa Mungu kuighadhabikia dhambi? (Kweli kabisa. Dhambi iliichafua/iliiharibu mbingu. Dhambi iliuharibu Uumbaji wa Mungu hapa duniani. Dhambi ilisababisha Yesu aingie kwenye suala kubwa la kafara na mateso. Mungu anapaswa kuchukia dhambi.)

E. Soma Warumi 5:1-2. Je, hii ni aina gani ya amani? (Mungu anachukia dhambi. Tunapohesabiwa haki kwa imani (yaani pale ambapo haki ya Yesu inapokuwa haki yetu), hii inashughulikia tatizo sugu ambalo Mungu analichukia.)

F. Je, hii inapendekeza kuwa tunapaswa kuwa na mtazamo wa aina gani dhidi ya dhambi? Mtazamo wa aina gani dhidi ya Mungu? (Kwa vile dhambi ingetuua kama Yesu asingeingilia kati, basi tunatakiwa kuichukulia kwa dhati. Ukweli kwamba tuliepuka kulipa adhabu ya dhambi haiifanyi dhambi kuwa na umuhimu wa chini. Ukweli kwamba Yesu aliacha vyote, na kufa kifo cha kutisha kwa ajili yetu unapaswa kutufanya kumshukuru milele!)

IV. Mtazamo wa Kibaka

A. Soma Warumi 1:16. Paulo anapoandika kuwa haionei haya injili, je, hiyo inakuambia kitu gani? (Kwamba kuna sababu ya kuwa na haya. Kama ulikuwa na mwanamke mrembo sana au mume mzuri sana, je, kamwe usingesema, “Sioni haya jinsi ambavyo mwenza wangu anavyoonekana?” Hapatakuwepo na sababu ya ukanaji.)

1. Je, kuna sababu gani iliyopo ya kuionea aibu injili? (Angalia kile kinachofuatia ambacho Paulo anakisema, “ni uweza wa Mungu.” Hiyo ndio alama/ishara yetu. Mungu wetu alikufa. Alisulubishwa na serikali. Hii inaonekana kuonyesha upungufu wa uwezo kwa upande wa Mungu, na hili ni suala la aibu.)


2. Je, usulubishaji unaonyeshaje uweza wa Mungu? Je, huu ni uweza wa aina gani? (Uweza wa Mungu ni upendo. Uweza wa Mungu ni kujitoa kafara yeye mwenyewe. Mungu alijeruhiwa ili kwamba tuweze kuokolewa. Kinachoonekana kuwa ni maelezo ya upungufu wa uweza kimsingi ni uthibitisho wa uweza wa upendo wa Mungu.)

B. Soma Warumi 1:17. Je, haki ya Mungu inayofunuliwa kwenye injili ni ipi – injili ambayo kwa juu juu ni ya aibu? (Kinachofunuliwa ni kwamba Mungu anaishinda dhambi kwa upendo. Hii “haki” inaishinda dhambi. Inatutoa kutoka kuwa watumwa hadi kuwa watu wenye haki.)

1. Je, tunaipataje hii haki? (Inaonekana kuwa kinyume sana na njia za ulimwengu. Lazima tuikubali kwa imani.)

C. Soma Yohana 3:16-18. Je, msingi wa upendo ni kujitoa kafara mwenyewe? (Ndiyo.)

1. Kwa nini Munghu alipaswa kujeruhiwa? (Kumbuka kwamba dhambi inasababisha kifo. Tunapaswa kufa kwa ajili ya dhambi zetu. Biblia inatuambia kuwa Mungu alikubali kwa hiari “kushindwa,” alikubali kufa kwa hiari kwa ajili yetu kwa sababu alitupenda. Hii inaonyesha kuwa Mungu sio mbinafsi. Kwamba alitupendelea sisi zaidi ukilinganisha na hadhi yake au starehe yake.)

V. Ghadhabu ya Mungu

A. Soma Warumi 1:18-19. Je, Mungu hana furaha? (Ameghadhabika!)

1. Je, Mungu ana sababu ya kutokuwa na furaha? (Hebu angalia mafungu ya Biblia ambayo tumeyapitia hivi punde. Mungu alikwenda mbali sana (alichukua hatua ndefu na za kushangaza) katika mchakato wa kutuokoa. Aliacha kila kitu ili aweze kuwaokoa wale waliomkataa.)

Je, unajisikiaje pale ambapo wale uliowapenda na kuwajali wanapokukataa?

2. Je, ghadhabu ya Mungu inajionyesha dhidi ya nani? (Dhidi ya wale wasio na Mungu na waovu.)

3. Je, sababu ya ghadhabu ya Mungu ni ipi? (Hawa watu wanaukandamiza ukweli.)

B. Soma Warumi 1:20. Je, hawa wakandamizaji wa ukweli wana kisingizio? (Hapana. Asili na uweza wa Mungu vi dhahiri tangu uumbaji. Tunaweza kuona kuwa Mungu yupo na tunaweza kuona kuwa tatizo la dhambi lipo.)


C. Soma Warumi 1:21-22. Je, ni kwa njia gani unaweza kukandamiza ukweli wa Mungu? (Njia nyingi, lakini Mungu anaonyesha njia mbili. Kwa kukana au kugeuza/kubadili kile ambacho Yesu ametutendea. Kwa kukana na kuwakilisha vibaya upendo wa Mungu. Kwa kutokumtukuza Mungu au kwa kutokumshukuru yeye.)

Hebu turejee kwenye lile suala la “haya/aibu.” Kama tunafedheheshwa kuhusu Mungu wetu na ujumbe wetu, je, sisi tu waovu? (Tunaukandamiza ukweli kwa kutompatia Mungu utukufu na kutokuwa na shukrani kwa kile alichotutendea pale msalabani.)


Rafiki, tulianza kwa kukiri kuwa sisi ni vibaka. Kwa sababu kamwe hatukutakiwa kulipa gharama, inawezekana tusizichukulie njia zetu za kiovu kwa dhati. Kisa cha injili kinatusaidia kuzichukulia njia zetu za kiovu kwa dhati. Kinatufunulia upendo mkubwa wa Mungu usio na ubinafsi na njia zetu za kibinafsi. Je, utadhamiria hivi leo kutenda kile kinachompendeza Mungu? Kuonyesha uelewa wako wa kafara yake na upendo wake kwa kugeuka na kuyaacha yale mambo yaliyomsababishia Yesu maumivu makali? Kwa kumpa Mungu utukufu kwa kile ambacho amekutendea?

Juma lijalo: Mungu wa Neema na Hukumu.

Friday, January 6, 2012

Somo la 2: Hapo Mwanzo

Somo limetafsiriwa na Mgune Masatu

(Mwanzo 1-3, Ayubu 38, Warumi 5)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: Juma lililopita niliandika kuwa huwezi kuwa Mkristo kama huamini katika Utatu Mtakatifu. Hapo nilimaanisha kuwa Mkristo lazima aamini kuwa Yesu ni Mungu kamili. Juma hili tunajifunza fundisho jingine la msingi kabisa la Biblia – kwamba Mungu alitamka na dunia ikawepo. Dunia haikuibuka, na Mungu “hakusimamia” masuala ya bahati kutokea na matukio ya kiasili. Je, ni kwa njia gani imani katika Uumbaji inahusika? Hebu tuzame kwenye Biblia zetu na kubaini zaidi!

I. Maelezo ya Mungu ya Mianzo

A. Soma Mwanzo 1:1-5. Je, Biblia inasema kuwa nani aliyeumba “mbingu na nchi?” (Mungu!)

1. Ujumbe wa msingi wa Mungu ni kwamba yeye ndiye Muumba. Lakini, ana ujumbe wa pili kuhusiana na kazi yake ya uumbaji. Je, ujumbe huo ni upi? (Hakuhitaji msaada wowote. Alianzia kwenye “ukiwa na utupu” na akatamka tu na ulimwengu ukawepo. Hakuhitajika “kuinua kidole.”)

B. Angalia tena Mwanzo 1:5. Je, ilimchukua Mungu muda gani kutenda hili? (Biblia inasema kuwa siku moja. Kama tungetakiwa kutafsiri hii “siku” kama kipindi kirefu cha muda, Mungu anaelezea siku kwa namna ambayo sote tunaielewa kutokana na uzoefu.)

1. Kwa nini Mungu anaziita “jioni” na “asubuhi” kuwa ni siku? Katika Mambo ya Walawi 23:32 tunaona kwamba kuanzia jioni hadi jioni ndicho kipimo cha siku. Tatizo linakwisha kama utasema kuwa “jioni” ni usiku (giza) na “asubuhi” ni mchana (nuru). Hiyo ndio siku kamili kwa kutumia jua likitumika kiuzoefu kama kipima muda.)

2. Vipi kuhusiana na ukweli kwamba jua bado halikuwepo, lakini baadaye liliumbwa (Mwanzo 1:16)? (Mungu anatumia kipima muda chenye uwiano sawa katika juma kabla na baada ya uumbaji wa jua. Lazima Mungu atakuwa aliumba jua bandia – hili sio tatizo kwa mtu anayeweza kuumba jua halisi!)

II. Kwa Nini Uumbaji Unahusika Sana kwa Mungu


A. Watu wengi wananukuu Ayubu 13:15 kusema kwamba Ayubu angekuwa mwaminifu kwa Mungu hata kama Mungu angemuua. Ukisoma sura yote (Ayubu 13) kile ambacho Ayubu anakisema ni kwamba “Ningependa kumshitaki Mungu kwenye mahakama ya mbinguni. Mungu atapaswa kuniletea mashtaka dhidi yangu na nitakuwa na fursa ya kujitetea. Nikipata kusikilizwa kwa haki, basi nitashinda. Nisiposhinda, basi nitasalia kuwa kimya na nitakufa.” Hiyo ndio sababu ambayo sehemu ya pili ya Ayubu 13:15 inasema kuwa, “nitaithibitisha njia yangu mbele zake.” Ayubu anampa Mungu changamoto. Soma Ayubu 38:1-3. Je, Mungu anaijibuje changamoto ya Ayubu? (Anasema kuwa, “nitakuuliza neno! Ewe mwanadamu mpumbavu, nitakutaka unijibu maswali machache.”)

1. Soma Ayubu 38:4-6. Je, majibu kwa maswali ya Mungu ni yapi? (Ayubu hakuwa shahidi.)

a. Je, ni swali gani hasa analoliuliza Mungu? (Wewe ni nani hata umpe changamoto Muumba?)

B. Pitia kwa haraka haraka sura yote ya Ayubu 38. Je, dhana ya Mungu ni ipi? (Kwamba yeye ni muweza wa yote na ana maarifa yote yanayohitajika. Uumbaji unatokea kutokana na kanuni na Mungu ndiye aliyeziumba kanuni.)

1. Je, uumbaji una umuhimu gani kwa madai ya Mungu kuwa yeye ni Mungu wetu? (Hii inaingia kwenye kiini cha suala lenyewe. Katika Biblia Mungu ananukuu kwa kurudia rudia Uumbaji wake kama msingi wa madai yake ya mamlaka juu ya Ayubu (na mtu mwingine yeyoye yule). Mjadala wa Uumbaji dhidi ya uibukaji unahusu uwezo na mamlaka ya Mungu. Mungu anatangaza kuwa “Mimi nina uwezo mkubwa kiasi kwamba nilitamka tu na kitu kikatokea.” Kimsingi, uibukaji unadai kuwa Mungu alihitaji msaada mkubwa na muda mwingi sana.)

C. Soma Mwanzo 1:26-27. Je maelezo haya yanakinzana vipi na nadharia ya uibukai? (Tulifanywa kwa mujibu wa ubunifu. Mungu alibuni kwamba wanadamu wanapaswa kuumbwa kwa sura na mfano wake. Mungu alibuni kwamba wanadamu wanapaswa kuwatawala wanyama.)

1. Je, kwa nini hili ni muhimu kwa Mungu? (Mungu ana uhusiano maalum na wanadamu. Hakujikwaa kwetu alipokuwa akitembea.)

2. Fikiria kwa muda mfupi kuhusu kile ambacho Biblia inakisema kuhusu uhusiano kati ya wanadamu na wanyama na uniambie kama uhusiano huo unakinzana na nadharia ya uibukaji? (Uibukaji unasema kuwa wanadamu sio tu kwamba walitokana na wanyama, bali pia matukio ya asili kwa kiasi kikubwa yalikuwa ni matokeo ya muingiliano na wanyama. (Ikimaanisha kwamba aidha tuliwashinda kwa mbio au tulikuwa werevu zaidi (tuliwashinda kwa akili) ya wanyama au tulikufa.) Biblia inasema kwa utofauti mkubwa kwamba “tuliwatawala” wanyama.)

D. Soma Kumbukumbu la Torati 30:19-20. Katika nadharia ya uibukaji, je, ni nani aliye mbunifu wa kweli wa wanadamu? (Mauti. Tulibuniwa na kifo. Kama kifo ndicho mbunifu wetu, basi Mungu alitudanganya kuhusu uchaguzi wa msingi sana aliouweka mbele yetu.)

E. Soma Mwanzo 3:1-4. Fungu hili pamoja na fungu tulilolisoma hivi punde katika Kumbukumbu la Torati linatuashiria kwenye kitu cha msingi sana kinacholeta mantiki. Je, ni “kisa” gani cha jumla ambacho Mungu anatuelezea kumhusu yeye na sisi? (Kwamba alituumba tukiwa wakamilifu. Hatukumtumaini, hatukumwamini na hatukumtii Mungu, na matokeo yake tukajiingiza kwenye utumwa wa unyonge, magonjwa na mauti ya milele.)

1. Je, ni kisa gani cha jumla ambacho nadharia ya uibukaji inatufundisha? (Kwamba tulitoka kwenye unyonge hadi kuwa wakakamavu na kuwa mnyama mwenye umiliki mkubwa – na kwa hiyo tukastahili kuwa na maisha bora zaidi!)

2. Je, hivi “visa” viwili vinaendana?


3. Je, unaweza kuhusianisha neema na matendo kwenye huu mchakato wa mawazo yenye mantiki? (Ndiyo! Biblia inasema kuwa uumbaji na ukombozi wetu ulitokana na neema na uwezo wa Mungu usiokuwa na mipaka. Uibukaji ni njia ya “matendo” ya kuupata wokovu na uzima. Tunaimarika kutokana na juhudi zetu wenyewe.)

F. Rafiki, unaweza kuona kuwa uibukaji unamvua Mungu utambulisho wake na kupindua kisa chake?

III. Kwa Nini Uumbaji Unahusika Sana kwa Wanadamu

A. Huenda sababu ya msingi sana ya kwa nini Uumbaji unahusika sana kwa wanadamu ni kwamba unasema kuwa tulitoka mikononi mwa Mungu. Lakini mitazamo yetu mingi ya msingi kuhusiana na maisha inahusianishwa moja kwa moja na mchakato mzima wa Uumbaji. Soma Mwanzo 2:20-23. Hoja moja inayosema kwamba “Mungu alisimamia uibukaji” ni kwamba waandishi wa Biblia hawakuweza kuelezea kwa uzuri kabisa mbinu za uibukaji, na kwa hiyo walielezea kisa ambacho kiliwasilisha wazo lililo sawa na uibukaji. Je, hoja hiyo inakubaliana na fungu la Biblia? (Hapana! Mungu ana maelezo ya kina sana. Undani wa taarifa anaoutoa unakinzana kabisa na wazo la masuala ya bahati na yale ya asili.)

1. Je, dhana hii inatuambia nini kuhusiana na uhusiano kati ya wanaume na wanawake? (Kwamba waliumbwa ili wawe sawa. Hawa alitoka ubavuni na sio kichwani au kwenye mguu wa Adamu.)

a. Je, uibukaji unatufundisha nini kuhusu uhusiano kati ya wanaume na wanawake? (Kwamba yeyote anayeweza kutawala anapaswa kufanya hivyo.)

B. Soma Mwanzo 2:24. Je, ndoa na uumbaji vinahusianishwaje? (Kama uibukaji ndio maelezo sahihi ya asili ya mwanadamu, basi ndoa ya “mwili mmoja” kati ya mwanamume na mwanamke haina maana yoyote.)

1. Soma Waefeso 5:28-31. Je, suala la “mwili mmoja” linatufundisha nini kuhusiana na jinsi ambavyo wanawake wanapaswa kutendewa kwenye ndoa?

C. Soma tena Mwanzo 3:2-4. “Utawala wa sheria” ni wa muhimu sana kwa jamii iliyo huru. Wanadamu wanapaswa kutawaliwa kwa sheria, sio mawazo holela ya mtawala. Je, mjadala wa uumbaji dhidi ya uibukaji unatufundisha nini kuhusiana na utawala wa sheria? (Mungu alituumba ili tutawaliwe kwa sheria. Anaamini (na aliifia) katika utawala wa sheria. Uibukaji unatoa hoja kukubaliana na wazo kwamba mtu mwenye uwezo kuliko wote ndiye anayeweka sheria.)

D. Soma Mwanzo 2:2-3. Je, Sabato inahusianaje na dhana nzima ya Uumbaji? (Ni sherehe na ukumbusho wa kila juma wa siku sita halisi za uumbaji. Kama vile kwenye ndoa, nguzo/uimara wa Sabato unaondolewa na nadharia ya uibukaji.)

E. Soma Warumi 5:12-15. Je, Paulo anaielezeaje injili? (Kwamba Adamu alituingiza dhambini na Yesu alituokoa kutoka dhambini. Yesu alishinda ilhali Adamu alishindwa.)

1. Vipi kama kamwe Adamu hakuwepo? Je, hiyo ingefanya nini kwenye mtazamo wetu wa wokovu?

F. Soma 1 Wakorintho 15:23-26. Je, ujumbe huu ni sehemu ya muhimu sana ya injili? (Ndiyo. Kwamba Yesu anashinda dhidi ya dhambi na anatuokoa kutoka kwenye mauti.)


1. Utabaini kwamba kifo ndio “adui wa mwisho,” na kinaangamizwa na Yesu. Je, kifo ni cha muhimu kwa namna gani kwenye nadharia ya uibukaji? (Ni suala zito. Utokeaji wa vitu kwa kufuata asili unawachukulia washindi na washindwa kama matokeo ya kifo.)

G. Soma Ufunuo 21:1-4. Kama huamini maelezo/dhana ya Mungu ya uumbaji wa asili, je, ni kwa nini sasa uamini maelezo yake ya uumbaji mpya?

1. Kama tunaamini kuwa dhana ya uumbaji ni analojia inayoelezea uibukaji, je, hiyo inatufundisha nini kuhusiana na makao yetu mapya ya mbinguni? (Angalia fungu la 4 – kwamba vitu vilivyoishia mbinguni ni vya msingi kwenye uibukaji, wenye nguvu ndio watakaoishi na wanyonge watakufa! Nadharia ya uibukaji haiendani kabisa na injili.)

H. Leo tumegusia tu matatizo ya uibukaji yakiwa ni maelezo ya mianzo (asili). Rafiki, kama umeikubali nadharia ya uibukaji kama maelezo ya kweli ya asili ya wanadamu, je, utatupilia mbali fikra hiyo na kuijenga imani yako kwenye kauli za asili za Mungu na mpango wake wa injili?

IV. Juma lijalo: Mungu Kama Mkombozi.

Wednesday, January 4, 2012

Somo la 1: Nafsi Tatu Katika Umoja

Somo limetafsiriwa na Mgune Masatu

(Kumbukumbu la Torati 6:4, Mathayo 26:63-64, Wakolosai 2:13-15)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2011, Bruce N. Cameron, J.D. Marejeo yote ya maandiko yametoka kwenye tafsiri ya New International Version (NIV), copr. 1973, 1978, 1984 International Bible Society, isipokuwa kama itaelezwa vinginevyo. Nukuu kutoka kwenye tafsiri ya Biblia ya NIV inatumika kwa ruhusa ya Wachapishaji wa Biblia wa Zondervan. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Kama huwa una kawaida ya kupokea somo hili kwa njia ya barua pepe na hukulipata kwa juma moja, unaweza kulipata kwa kubofya kwenye www.lesoni.blogspot.com kwa lugha ya Kiswahili na http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: Nilipoanza kutumia kompyuta kwa kweli ilikuwa inanichanganya sana. Nilitaka kujua jinsi zinavyofanya kazi (kwenye sehemu zake za mashine). Mtu yeyote anaweza kuandika na kuchapa nyaraka, kama vile jinsi ambavyo mtu yeyote anavyoweza kuendesha gari. Lakini je, nini kinachotokea “chini ya zulia?” Ili kujibu swali hilo nilisoma sana vitabu na, kwa maelekezo ya mwanangu mdogo, nilitengeneza kompyuta. Sasa nimeridhika kuwa ninafahamu vitu vya msingi hata kama maarifa yangu bado siyo makubwa sana (hayajakamilika). Somo letu juma hili linafanana na hilo. Tutajifunza vitu vya msingi kumhusu Yesu na Utatu Mtakatifu, lakini maarifa kamili kuhusiana na hayo ni zaidi ya upeo/ufahamu wetu. Kwa sababu sidhani kama unaweza kuwa Mkristo bila kuwa mfuasi wa Utatu Mtakatifu, basi hebu tuzame kwenye Biblia zetu na kuona kile tunachoweza kujifunza!

I. Fumbo/Kitendawili

A. Soma Kumbukumbu la Torati 6:4-5 na Marko 12:28-30. Je, hii inatuambia nini kumhusu Mungu? (Kwamba “Bwana ni mmoja.”)

1. Je, unadhani ni kwa nini Mungu anaanzisha amri ya “unipende kwa moyo wako wote” na kauli ya “Bwana ni mmoja?” (Kumpenda Mungu kwa ukamilifu ni amri chanya, na kutoipenda miungu mingine ni amri hasi.)

2. Tafsiri Mpya ya Biblia inatuambia kuwa Kumbukumbu la Torati 6:4 ni “ombi la msingi katika dini ya Kiyahudi.” Inaitwa kuwa “Shema” kwa sababu inaanza na neno “sikiza,” neno ambalo ndilo linalomaanishwa na neno shema kwa Kiebrania. Kama hili ndilo lililokuwa ombi la msingi la dini ya Kiyahudi, je, inapaswa kumaanisha nini kwetu tunaoamini katika uvuvio wa Agano la Kale?

B. Je, uligundua kuwa alikuwa ni Yesu ambaye aliyarudia yale maneno katika Marko 12:29 kwamba Mungu ni “mmoja?” Wayahudi na Waislamu wanasema kuwa Wakristo hawamwamini Mungu mmoja (wale wanaoamini katika Mungu mmoja) kwa sababu tumaanini kwamba Mungu Baba, Roho Mtakatifu na Yesu wote ni Mungu. Kama Wayahudi na Waislamu wapo sahihi, kwa nini Yesu avute usikivu kwa Shema na kusema kuwa amri ya upendo “ni ya muhimu kuliko zote?”

C. Hivi karibuni, kitabu kilichouzwa kwa mauzo ya juu kabisa (ambacho pia kiliigizwa sinema) kilielezea kisa kilichoegemea kwenye wazo kwamba Kanisa Katoliki lilipindisha injili ili kuifanya ionekane kuwa Yesu alidai kuwa yeye ni Mungu, wakati ambapo kimsingi Yesu hakuwa na hayo madai. Je, injili ndizo chanzo pekee cha madai ya kwamba Yesu ni Mungu?

II. Msingi wa Utatu Mtakatifu


A. Soma Mwanzo 1:1-2. Mungu alipojitambulisha katika Biblia, je, alifunua nini kuhusu asili yake? (Alifunua kwamba “Mungu mmoja” alikuwa na “Roho!” Kwa hiyo, tangu mwanzo kabisa wa utangulizi wake Mungu anatujulisha kuwa yupo na anaye Roho Mtakatifu ambaye pia yupo.)

B. Soma Mwanzo 1:26-27. Je, hili suala la “na tumfanye mtu kwa mfano wetu” ni kitu gani? Je, hii inapendekeza nini kuhusu Mungu? (Kwamba yeye ni “uwingi” wa namna fulani hivi.)

1. Angalia tena fungu la 27. Je, hiyo inapendekeza nini kuhusu asili ya Mungu? (Kwamba inajumuisha “mwanamume na mwanamke.”)

2. Hebu tusome Mwanzo 2:22-24. Je, ni kitu gani ambacho Mungu anakiita kuwa “mwili mmoja?” (Adamu na Hawa, na wale wote wanaooana baada ya hapo.)

C. Je, mafungu haya kutoka katika kitabu cha Mwanzo yanatufunulia nini kuhusu mtazamo wa Mungu wa neno “mmoja?” (Kwamba ana mtazamo mpana wa neno “mmoja!” Adamu na Hawa walikuwa na haiba yao wenyewe, lakini Mungu aliwaita “mwili mmoja.” Tangu mwanzo kabisa, Mungu anafunuliwa kuwa na Roho “anayetulia juu ya uso wa maji.” Unaweza kusema kuwa Mungu ni Roho tu, lakini hiyo haiendani sana na kauli iliyofuatia ya “na tumfanye mtu kwa mfano wetu.” Tunaweza kuona kuwa Msingi wa Utatu Mtakatifu haukuanzia kwenye injili, badala yake ulianzia katika kitabu cha Mwanzo.)

D. Soma Waamuzi 3:9-10 na Waamuzi 6:34. Je, hii inakukumbusha juu ya kile unachokiona mara kwa mara katika Agano Jipya? (Ndiyo. Agano Jipya linaendeleza wazo la Roho wa Mungu kuwa kitu kilicho tofauti na Yesu na Mungu Baba. Tunaona kitu cha aina hiyo hiyo katika Waamuzi.)

III. Madai ya Yesu ya Uungu/Umungu

A. Kwenye utangulizi, nilisema kuwa mtu sio Mkristo kama haamini katika Utatu Mtakatifu. Je, hiyo ni kauli isiyokuwa ya haki? Hebu tusome Yohana 8:58. Je, madai ya Yesu ni yapi hapa?

B. Soma Yohana 6:35-40 na Yohana 6:51. Je, madai ya Yesu ni yapi hapa?

C. Soma Yohana 8:12. Je, madai ya Yesu ni yapi hapa?

D. Soma Yohana 11:25-27. Je, madai ya Yesu ni yapi hapa?

E. Soma Yohana 10:30. Je, madai ya Yesu ni yapi hapa?

F. Soma Yohana 10:32-33 na Luka 5:21-24. Je, wasikilizaji wa Yesu walielewa kuwa madai ya Yesu yalikuwa yapi?

G. Soma Marko 14:61-62. Je, Yesu analeta madai gani hapa?

H. Soma Mathayo 3:16-17. Je, hii inatufundisha nini kuhusu Utatu Mtakatifu?

I. Soma Yohana 1:1-4 na Yohana 1:14. Je, hii inatufundisha nini kumhusu Yesu?


IV. Kwa Nini Inajalisha

A. Kwenye haya mafungu uliyoyasoma hivi punde Yesu kwa wazi kabisa anaudai Uungu. Anajiita mwenyewe kuwa “MIMI NIKO AMBAYE NIKO!” Hivi ndivyo ambavyo Yehova anavyojielezea (Kutoka 3:13-14). Kama Yesu sio Mungu, je, hii inasema nini kumhusu yeye? (Kwamba yeye ni mwongo au mlaghai. Yeye sio wa kuaminiwa, achilia mbali kuabudiwa.)

1. Soma Zaburi 73:7-9 na Yeremia 23:34. Je, mafungu haya ya Agano la Kale yanatuambia nini kuhusu madai ya uongo? (Yanatoka kwa mwovu.)

B. Soma Mathayo 26:63-64. Upeo wote wa Agano la Kale ni kuhusu kafara ya mwanakondoo kwa ajili ya dhambi ya wanadamu. Watu wa Mungu walimtarajia Masihi aje na kuwakomboa. Je, Kuhani Mkuu anamuuliza Yesu kama yeye ni Masihi? (Ndiyo. Yesu anadai kuwa yeye ni Masihi – Masihi aliyeahidiwa ambaye anatoka kwa Mungu, atarejea kwa Mungu na atakuja tena kuwakomboa watu wake.)

C. Soma Yohana 8:23-30. Je, Yesu anafundisha kitu gani ambacho ni suala nyeti linapokuja suala la uungu wake? (Tutakufa dhambini mwetu! Yesu anatuambia kwa dhahiri kabisa kwamba kama tusipomkubali yeye kama Masihi, Kristo, Mwana wa Mungu, basi hatuna Masihi, hatuna Mwanakondoo wa Mungu, na tutakufa kwa ajili ya dhambi zetu! Suala linaweza lisiwe tete zaidi au la msingi zaidi kwenye tumaini letu kama Wakristo!)

V. Kwa Nini Paulo Anadhani Kuwa ni Muhimu

A. Kumbuka kitabu maarufu na sinema iliyohoji ujinga wa Biblia kwamba Yesu hakufikiri kuwa alikuwa na uungu – kwamba hili ni jambo ambalo lilibuniwa baadaye na Kanisa Katoliki ili kuunga mkono umuhimu wake? Tumeona kwamba msingi wa Utatu Mtakatifu unapatikana katika kitabu cha Mwanzo, na tumeona kuwa Yesu alidai kuwa yeye ni Mungu na Masihi. Hebu tuangalie kile ambacho Paulo aliandika kumhusu Yesu na uungu wake. Soma Wakolosai 2:9-10. Je, Paulo ansema nini kuhusiana na Uungu wa Yesu?

B. Soma Wakolosai 2:13-15. Je, Paulo anasema nini kumhusu Yesu kama Masihi azichukuaye dhambi zetu? (Hivyo ndivyo ambavyo Paulo anavyomwelezea Yesu.)

VI. Kwa Nini Petro Anadhani Kuwa ni Muhimu

A. Soma Matendo 1:1-5. Je, maelekezo ya Yesu kwa wafuasi wake kwa ajili ya siku zijazo ni yapi?

B. Soma Matendo 2:1-4. Je, hiki ndicho alichokiahidi Yesu?

C. Soma Matendo 2:29-36. Je, Petro anasema nini kumhusu Yesu?

1. Je, Petro anadai kuwa ni nani aliye chanzo cha kauli yake? (Roho Mtakatifu.)


D. Rafiki, kitabu cha Mwanzo kinaweka msingi wa Utatu Mtakatifu. Yesu anadai kuwa Masihi na “MIMI NIKO AMBAYE NIKO.” Petro na paulo wanadai kuwa Yesu ni Masihi – na Petro ansema kuwa kauli hii inatokana na uvuvio wa Roho Mtakatifu. Agano Jipya, kwa ujumla wake, linatoa hoja yake kuwa Yesu ni Mungu. Agano la Kale linamtaja Yesu kama Masihi. Hili sio suala la kughushi/kubuni la viongozi wa awali wa kanisa kutaka kujiongezea umaarufu/umuhimu wao. Huu ni ujumbe wa msingi wa Biblia. Kama hatukiri/hatukubali kuwa Yesu ni Mungu na kwamba alikufa badala yetu kwa ajili ya dhambi zetu, basi tumepotea. Je, utakubali hivi leo kwamba Yesu ni Bwana wetu na Mungu wetu?

VII. Juma lijalo: Hapo Mwanzo.