Thursday, December 23, 2010

Robo ya Kwanza 2011 - Somo la 1: Hisia

Ndugu msomaji, juma hili tunaanza mfululizo mpya wa mwongozo wetu wa kujifunza Biblia katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2011 (Januari - Machi). Karibuni tuendelee kujifunza sote kwa uongozi wa Roho Mtakatifu.


Somo la 1: Hisia
(Wagalatia 5, Wakolosai 3, 2 Samweli 13)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: Je, Biblia inaonekana kuwa mahala pazuri pa kujifunza kuhusu hisia za kibinadamu? Angalia Wagalatia 5:22-23 inayosema kuwa “tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema na kiasi. Je, ni mangapi kati ya hayo matunda aidha ni hisia au yanalinganishwa kwa karibu kabisa na hisia? Mtu yeyote aliyekwishasoma kitabu cha Robert Whitaker kinachoitwa Anatomia (Sayansi ya mwili) ya Magonjwa ya Mlipuko ana mashaka makubwa ya kuirejea sayansi katika kuponya matatizo ya kihisia na ya kiakili. Kitabu chake kinaelezea ukweli kuwa katika nchi ya Marekani tuna ongezeko kubwa la watu wanaodhoofishwa na hisia zililoanzia kwa kuanza kwa matumizi ya dawa katika kuponya matatizo ya kiakili. Hoja yake ni kwamba kutumia dawa za sasa ni kama kutupa mawe/miamba kwenye mitambo ya kisasa. Dawa ni kwamba tu zinafanya tatizo kuwa kubwa zaidi. Ikiwa sayansi yaweza kutoa majibu au la, mimi sina wasifu wa kuzungumzia hilo. Lakini hebu tuzame kwenye mfululizo wetu wa kujifunza ili kuona kuwa ni majibu gani yanapatikana kwenye Biblia!


I. Wajibu Wako Kwenye Hisia Chanya

A. Soma Wagalatia 5:16-17. Je, unateseka na mgogoro/mtafaruku wa kihisia? Je, mara nyingine hisia zako hazidhibitiki au sivyo ambavyo ungetaka ziwe?

1. Je, ni mgogoro gani ambao Paulo anatufundisha ulio uzoefu wa kila mwanadamu? (Paulo anatuambia kuwa asili yetu ya dhambi inataka kufanya jambo moja na Roho Mtakatifu anatutaka tufanye jambo jingine. Mambo haya mawili yapo katika mgogoro kiasi kwamba tunajikuta tukifanya mambo tusiyotaka kuyafanya.)

2. Je, nini kilicho ufunguo cha maisha sahihi? (Kuishi maisha yanayoongozwa na Roho Mtakatifu.)

B. Soma Wagalatia 5:19-21. Katika orodha hii ambayo Paulo anaiita “matendo ya asili ya dhambi,” je, unaona hisia zozote? (Ndiyo.)

1. Je, mchanganyiko huu unapendekeza nini? (Unapendekeza kuwa hisia hasi ni sehemu ya asili yetu ya asili ya dhambi. Tunazipata bila kuziomba! Pili, inapendekeza kuwa hisia hasi zina aina fulani hivi ya muunganiko na matendo hasi.)

C. Soma Wagalatia 5:22-25. Tumejadili kwenye utangulizi kuwa hizi ni hisia au zinalinganishwa kwa karibu kabisa na hisia. Je, hizi ni hisia chanya, hisia ambazo ungetaka ziwe sehemu ya maisha yako?

1. Je, tunapataje hizi hisia? Au, je, zipo nje kabisa ya uwezo wa uchaguzi? (Uchaguzi ni kigezo. Kwanza, ni kigezo kwenye uchaguzi wetu wa “kuishi kwa mujibu wa Roho.” Pili, Paulo anatuambia kuwa tunaweza “kuisulubisha” asili yetu ya dhambi.)

2. Je, ni wangapi kati yenu mnapata ugumu kuishi kwa mujibu wa/kuendana na Roho na kuzisulubisha asili zenu za dhambi? (Kama wewe uko kama mimi, mkono wako umenyooshwa juu. Sina uhakika kwamba mafanikio ni rahisi, lakini nina uhakika kuwa Biblia inatufundisha kuwa uchaguzi ni kigezo katika hisia zetu za kibinadamu.)

D. Soma Wakolosai 3:5-10. Je, hisia ngapi hasi tunaziona ambazo zimeorodheshwa kwenye haya mafungu? (Kadhaa.)

1. Je, ni ushawishi gani tulionao dhidi ya hizi hisia hasi? (Paulo anatuambia “tujiweke mbali” nazo.)

E. Soma Wakolosai 3:12-14. Tunaona tena hisia chanya na pendekezo kuwa tuna ushawishi dhidi ya hisia zetu. Je, ni matendo gani mahsusi ambayo mafungu haya yanapendekeza ambayo tunaweza kuyafanya? (“Kuchukuliana” na “kusameheana.”)

1. Je, hizi ni chaguzi?

2. Baini kuwa Paulo anasema “upendo” utatufungamanisha kwenye umoja kamili. Je, tunaweza kuchagua kupenda? Au, je, hiyo ni hisia isiyodhibitika?

a. Hebu tuchukulie kuwa humpendi mtu fulani, lakini unataka kujifanya kumpenda. Je, unawezaje kulifanya hilo? (Utakuwa mwema kwa huyo mtu. Utakuwa mkarimu. Utamtendea mtu huyo kama ambavyo ungetaka kutendewa. Hiyo inaonekana kama “kuchukulia” na “kusamehe,” si ndio?)

(1) Je, hii ni tiba ya Kibiblia ya kutibu matatizo ya kihisia? (Kama wewe uko kama mimi, baadhi ya nyakati zangu za furaha sana ni pale ninapomsaidia mtu fulani naye anashukuru/anafurahia. Kuwa mwema na mwenye upendo kwa watu wengine ni kama ndege iliyojazwa mafuta kwa ajili ya hisia chanya. Kuwa mwema na mwenye kujali ni uamuzi. Hakupo nje ya utayari wa uhuru wa uchaguzi.)

II. Mfano wa Kibiblia

A. Soma 2 Samweli 13:1-2. Je, Amnoni anateseka na tatizo la kihisia? (Ndiyo. Ilimfanya augue kimwili.)

1. Soma Mambo ya Walawi 18:11. Je, fungu hili linasema nini kuhusu matamanio ya Amnoni? (Kwamba asingeweza kumwoa Tamari.)

B. Soma 2 Samweli 13:3-6. Je, Amnoni ana uchaguzi wa kufanya hapa kuhusu kuzilisha hisia zake hasi?

1. Je, hapa kuna usawia/ufananisho/uhusiano katika maisha yako? Je, unapambana na hisia hasi unazozilisha kwa chaguzi zako hafifu?

C. Soma 2 Samweli 13:9-11. Hadi kufikia hapa, je, ni chaguzi zipi mbaya ambazo Amnoni amezichagua? (Amedanganya ili kumleta Tamari katika chumba chake. Amemtoa kila mtu nje na sasa wapo yeye na Tamari peke yao. Sasa anaonekana kumlazimisha ili afanye nae ngono{amtenze/ambake}.)

D. Soma 2 Samweli 13:12-14. Je, hii dhambi ni ya bahati mbaya? Je, Amnoni ameonywa kikamilifu kuhusiana na asili ya dhambi yake? (Amnoni amekuwa akikimbilia kwenye aina zote za “taa nyekundu” kuelekea katika hii hatua ya chini. Ameruhusu hisia zake ambazo hakuziangalia kwa makini kuwa tabia mbaya ajabu.)

1. Soma tena Wakolosai 3:5. Je, badala yake Amnoni angetakiwa kufanya nini? (Paulo anasema kuwa hisia zilizosababisha kufikia katika hatua hii zinategemeana na uchaguzi wetu. Tuna uwezo wa “kuzifisha” hizi hisia.)

E. Soma 2 Samweli 13:15. Je, hapa Amnoni anateseka kutokana na matatizo ya kihisia?

1. Je, ni kwa kiasi gani sasa tunaweza kuona kwamba haya matatizo yanafungamanishwa na maamuzi yake mabaya?

F. Soma 2 Samweli 13:17-20. Je, hapa Tamari anateseka kutokana na matatizo ya kihisia?

1. Je, kuna kitu chochote ambacho angeweza kukifanya kwa utofauti ili kuepuka matatizo yake ya sasa ya kihisia? (Hapana.)

a. Je, mistakabali ya Amnoni na Tamari inatufundisha nini kuhusiana na ugumu/matatizo ya kihisia? (Baadhi ni matokeo ya chaguzi zetu hafifu, na baadhi yanakuja pasipo kuwa na kosa lolote tulilolitenda.)

G. Soma 2 Samweli 13:21-22 na 2 Samweli 13:28-29. Je, Absalomu anateseka kutokana na tatizo la kihisia?

1. Je, hili ni kosa lake?

2. Je, Absalomu angeweza kufanya nini ili kuepuka kuacha tatizo lake la kihisia kufikia hatua ya mauaji? (Wagalatia 5:20 inatuambia kuwa chuki/uadui ni sehemu ya asili yetu ya dhambi, na kuishi kwa mujibu wa Roho ni suluhisho la asili yetu ya dhambi.)

III. Maoni ya Yesu Juu ya Hisia

A. Soma Yohana 16:20. Kwenye somo letu la Biblia tumeona uhusiano/ulinganifu kati ya hisia njema na kuishi maisha yanayoongozwa na Roho Mtakatifu. Je, fungu hili linapendekeza nini kuhusu huo uhusiano/ulinganifu? (Ulimwengu, unaodhaniwa kuwa hauishi kwa mujibu wa Roho, unafurahia wakati wale wanaoongozwa na Roho wanahuzunika.)

1. Chungua/changanua muktadha wa Yohana 16:20. Je, unatoa mwanga gani kwenye kauli ya Yesu? (Sababu ya huzuni ni kwamba Yesu atatiwa mbaroni hivi karibuni na kusulubiwa.)

a. Je, hii inapendekeza nini kuhusiana na hisia za Kikristo na kibinadamu? (Kwamba mazingira yaliyo nje ya udhibiti wetu yatatusababishia huzuni – wakati ambapo ulimwengu unafurahia uovu.)

B. Soma Yohana 16:21-22. Je, mwisho wa tumaini la matatizo yetu ya kihisia ni upi? (Ni ya kitambo kidogo. Ni ya msingi katika mwanga/muktadha wa ukweli kuwa Yesu atakuja tena kutupatia furaha!)

C. Soma Mathayo 26:36-38. Je, Yesu anateseka kutokana na hisia ipi?

1. Tunapochukulia kwamba Yesu aliteseka hisia hasi, je, tuhitimisheje kuhusu matatizo ya kihisia na dhambi? (Ugumu/matatizo ya kihisia yanaonekana kufanana na magumu/matatizo mengine. Kwa ujumla, kuishi maisha yanayoongozwa na Roho hutupatia hisia chanya. Kuishi maisha yanayoongozwa na asili yetu ya kibinadamu hutupatia hisia hasi. Hata hivyo, tunaishi kwenye ulimwengu wenye uovu ukiwa na watu waovu – na wanaweza kutusababishia kuteseka kihisia. Ni hadi hapo Yesu atakapokuja tena, ndipo matatizo yetu, yakijumuisha matatizo yetu ya kihisia, yatakapoponywa.)

D. Rafiki, je, utadhamiria hivi leo kuboresha afya yako ya kihisia kwa kumwomba Roho Mtakatifu akuongoze maishani mwako? Kwa nini usimwombe sasa hivi?

IV. Juma Lijalo: Mpango wa Mbingu Kuhusiana na Wasiwasi.

0 comments:

Post a Comment