Thursday, December 30, 2010

Somo la 2: Msaada wa Mungu wa Kukabiliana na Wasiwasi

(Mwanzo 15, Yohana 14, Mathayo 6)

Somo hili limetafsiriwa kutoka katika Copr. 2009, Bruce N. Cameron, J.D. Majibu yaliyopendekezwa yanapatikana kwenye parandesi (kwenye mabano). Somo limekaa kimtazamo kwamba mwalimu anatumia ubao au sehemu nyingine yoyote ambayo inaweza kuonekana na wanafunzi. Somo hili pia linaweza kupatikana kutoka http://www.GoBible.org kwa lugha ya Kiingereza pamoja na lugha nyingine kama vile Kifaransa, Kijerumani. Omba kwa ajili ya uongozi wa Roho Mtakatifu unapojifunza.

Utangulizi: “Siku moja moja.” “Usijali, furahia,” “Unasema – Mie niwe na wasiwasi?” Ninafikiria hiyo kauli ya kwanza kama bango lililopachikwa kwenye gari, ya pili kama kaulimbiu ya kisiwa fulani hivi, na ya tatu ni nukuu kutoka kwa Alfred E. Neuman kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti la uchizi. Je, haya ni maneno ya kuishi kwayo? Au, je, ni fikra za watu wasio na njozi za kuona mbali, wavivu na wenye wazimu/ kwa ujumla, suluhisho langu kwenye wasiwasi ni kufanya kazi kwa bidii, kufanya mazoezi zaidi na kupanga vyema. Mimi ni kichaa? Je, unakabilianaje na wasiwasi? Je, wasiwasi unadhoofisha kabisa maisha yako na kuyafanya yawe na furaha kidogo? Hebu tuzame kwenye Biblia na kuona kile tunachoweza kujifunza kuhusiana na mtazamo wa Mungu juu ya wasiwasi!

I. Ibrahimu na Wasiwasi

A. Soma Mwanzo 15:1. Je, ni aina gani ya vitu ambavyo kwa kawaida huwa unakuwa na wasiwasi navyo? (Kutokewa na kitu kibaya kwako wewe au kwa familia yako?. Kufadhaishwa kwa kutotenda jambo fulani kwa uzuri.)

1. Kama majibu yaliyopendekezwa yanaakisi wasiwasi wako, je, ni kwa jinsi gani Mungu anayazungumzia? (Mungu anasema “mimi ni ngao yako” ambayo inapendekeza kuwa anatukinga kutokana na vitu vibaya. Mungu pia anasema kuwa yeye ni “thawabu yetu kubwa sana,” kitu kinachopendekeza kuwa tutakuwa salama. Tutapewa thawabu.)

B. Soma Mwanzo 15:2-3. Ibrahimu hasemi kuwa ana wasiwasi. Je, unadhani kuwa ana wasiwasi? (Mungu anasema nitakuwa ngao yako na thawabu yako. Ibrahimu anajibu kuwa Mungu hajamkinga kutokana na matatizo ya kifamilia ya kutokuwa na mrithi. Mungu hajamsaidia katika Idara ya thawabu kwa sababu hana mwana wa kuendeleza uzao wake na kurithi fedha zake. Kama hivi ndivyo vitu ambavyo kwa kawaida huwa tunakuwa na wsiwasi navyo, basi Ibrahimu ana wasiwsi.)

1. Je, wewe u kama Ibrahimu: je, unasema, (ahadi za Mungu haziendani na uhalisia?”

2. Je, una wasiwasi kuhusiana na kile unachokisoma kutoka kwenye Biblia? Kwa mfano, Ayubu, mtu mkamilifu, watoto wake wanauawa na anapoteza utajiri wake. Tunasoma vitu kwenye Biblia ambavyo vinapaswa kuwafanya wafuasi wa Mungu kuwa na vitu vingi vya kuwa na wasiwasi navyo (kama vitu hivyo vina mantiki yoyote), sawa?

C. Soma Mwanzo 15:4-6. Je, Mungu anajibuje swali la Ibrahim kuhusiana na pengo lililopo kati ya ahadi za Mungu na uhalisia? (Mungu anaweka ahadi maalum/mahsusi kwa Ibrahim kwamba ataziba pengo hilo siku za usoni – na Ibrahim anamwamini Mungu.)

1. Je, ni kwa namna gani tunapaswa kukitumia kisa hiki kivitendo maishani mwetu? (Ibrahimu aliangalia mbele zaidi ya uhalisia kwenye ahadi ya Mungu. Tunajua kuwa Mungu kwa hakika alitimiza ahadi yake kwa Ibrahim.)

2. Soma Waebrania 11:11&13. Je, ni mustakabali upi unaelezewa hapa kwa ajili ya wasiwasi? (Kuamini ahadi za Mungu hata kama hatuzioni zikitokea tungali hai.)

3. Je, unaweza kuipataje ahadi ya Mungu kwako? (Yumkini Mungu atatujia kama alivyomjia Ibrahim na kuweka ahadi mahsusi. Kwa namna hiyo hiyo, tunahitajika kuichungua Biblia kwa ajili ya ahadi za Mungu kuhusiana na vitu vinavyotutia wasiwasi. Hebu tufanye hivyo katika hatua inayofuata.)

II. Ahadi ya Mungu Kuhusu Mahusiano

A. Soma Yohana 14:1-3. Je, ni kitu gali kilikuwa kinawahangaisha wanafunzi wa Yesu? (Yesu aliwaambia kuwa alikuwa anaondoka.)

1. Je, ni aina gani ya wasiwasi ilisababishwa na hilo? (Wanafunzi wake walikuwa na wasiwasi kuhusiana na “familia zao.” Walikuwa na wasiwasi juu ya hatma ya taaluma yao siku za usoni (angalia Matendo ya Mitume 1:6).)

a. Je, wanafunzi walipaswa kuwa na wasiwasi kuhusiana na vitu hivi? Je, tunajua nini kuhusu siku zao zijazo ambazo wao hawakuzijua? (Ndoto zao za kuwa watawala hapa duniani zilivunjwa matumaini. Yesu hakurudi kuwachukua kwenda nyumbani katika kipindi cha maisha yao.)

2. Je, ni ahadi gani anayowapatia Yesu inayohusika kwetu? (Yesu alisema kuwa angeyafanya haya mambo sawia ambapo angerejea.)

III. Ahadi za Mungu Kuhusiana na Vitu

A. Soma Isaya 33:15-16. Je, Mungu anawaahidi nini waaminifu? (Maji ya kutosha na chakula cha kutosha.)

1. Je, wanafunzi walikuwa na malengo/matarajio makubwa ya kidunia zaidi ya hayo? Je, vipi kuhusu wewe?

a. Je, inawezekana kuwa baadhi ya wasiwasi wetu upo kwa sababu tunaweka matamanio yetu ya kuwa na vitu kuwa ya juu sana? Je, ulafi/uroho ni chanzo cha wasiwasi wetu?

2. Soma Wafilipi 4:11-13. Nini siri ya Paulo ya kuepuka wasiwasi kuhusiana na utajiri wake?

B. Soma Mathayo 6:25. Hii inapendekeza uwekaji wa vipaumbele vyetu kwa ajili ya matamanio yetu. Ni yapi hayo? (Uzima na afya njema ni vya muhimu zaidi ya chakula na mavazi.)

1. Je, huu mpangilio wa umuhimu unahimiliwa na wasiwasi? (Hehu tuendelee kusoma.)

C. Soma Mathayo 6:26. Je, tunapaswa kuhitimishaje kuhusiana na wasiwasi kutoka katika hili fungu? (Ya kwamba Mungu atatupatia chakula kwani anawapatia chakula ndege ambao ni wenye umuhimu mdogo.)

1. Rejea nyuma na uangalie mpangilio wa umuhimu: ya kwamba maisha yetu ni ya muhimu kuliko chakula. Je, Yesu anasema nini kuhusu maisha yetu? (Kama Mungu atatoa chakula, kwa hakika atatoa pia kwa ajili ya uzima wetu.)

2. Je, Yesu anapendekeza kuwa hatuhitajiki kupanda, kuvuna na kuhifadhi?

3. Je, umegundua nini kuhusiana na ndege na chakula: je, wanakaa na kuacha kucharuko (wanyama wadogo) wawalishe? (Kwa hakika ndege wanatafuta chakula. Wanakifanyia kazi chakula chao.)

a. Kwa vile mara zote ndege wanafanyia kazi chakula chao, lakini hawapandi, hawavuni au hawahifadhi, je, tunapaswa kuhitimishaje kuhusiana na Mungu wetu na wasiwasi wetu kuhusu chakula? (Mungu aliwapatia wanadamu mpango wa kupanda, kuvuna na kuhifadhi. Aliwapatia ndege mpango wa siku zote wa kutafuta chakula. Vyovyote iwavyo vile katika mpango wa utekelezaji, wasiwasi sio sehemu ya mpango kwa sababu Mungu ndie chanzo chetu cha mwisho.)

D. Soma Mathayo 6:27. Je, ni ukweli kwamba hatuwezi kuongezea urefu wa maisha yetu? Hivi karibuni rafiki yangu alipatwa na ugonjwa wa kisukari kwa kuwa alikuwa mnene sana. Muda mfupi kabla ya hapo alikuwa akivuta sigara. Mwanangu (ambaye ni daktari wa watu) alisema “Anapaswa kuwa na wasiwasi kuhusiana na urefu wa maisha yake. Atoe miaka kumi kwa ajili ya kisukari na miaka mingine kumi kwa ajili ya uvutaji wa sigara.” Je, rafiki yangu hapaswi kuwa na wasiwasi? (Angalia kwa makini katika kile alichokisema Yesu: wasiwasi hautakufanya uishi maisha marefu. Pia, haitakufanya uwe mrefu zaidi au uwe na mwonekano mzuri. Hata hivyo, rafiki yangu ataishi maisha marefu kama atapungua uzito na kuacha kuvuta sigara.)

E. Soma Mathayo 6:28-30. Je, ni malalamiko gani ambayo unayasikia mara kwa mara kutoka kwa Wakristo wenzako kuhusiana na uvaaji wa watu wengine? (Baini kuwa Yesu hahukumu nguo nzuri. Anahukumu wasiwasi juu ya kuwa na nguo.)

1. Kumbuka mjadala wetu wa kipaumbele. Je, Yesu anasema nini zaidi ya uvaaji? (Kwa kuwa miili yetu ni ya muhimu kuliko nguo (Mathayo 6:25), Yesu anatuambia kuwa hatuhitaji kuwa na wasiwasi kuhusiana na miili yetu pia.)

F. Soma Mathayo 6:31-32. Je, dunia inajishughulishaje na uhitaji wa chakula, vinywaji na mavazi? (Wanavifanyia kazi kwa nguvu sana. Je, hii inakukumbusha jinsi nilivyosema ninajishughulisha na wasiwasi – kuifanyia kazi kwa bidii?)

G. Soma Mathayo 6:33. Je, Wakristo wanapaswa kujishughulishaje kwenye uhitaji wa chakula, vinywaji na mavazi? (Badala ya kukimbilia kutafuta fedha, tunahitajika kukimbilia kuuendeleza Ufalme wa Mungu. Tunahitajika kuyaweka mbele maisha yenye haki. Hii haimaanishi kuwa hatufanyi kazi kwa bidii, inamaanisha kuwa na bidii yetu katika kuuendeleza ufalme.)

H. Soma Mathayo 6:34. Je, hii ni “mara moja moja?” au, je, hii ni “usipoteze furaha na utendaji mzuri wa siku kwa kuwa na wasiwasi kuhusu kesho?”

1. Tovuti ya Bible.org inatuarifu kutoka kwenye chanzo kisichojulikana kuwa wastani wa wasiwasi wa mtu unajielekeza kwenye: asilimia 40 vitu ambavyo kamwe havitatokea; asilimia 30 vitu ambavyo haviwezi kubadilishwa; asilimia 12 ukosoaji wa kizandiki wa watu wengine; asilimia 10 afya – ambao haitegemezwi na msongo; na asilimia 8 matatizo ya uhakika/ya kweli ambayo lazima yakabiliwe. Je, hii ni kweli kwa uzoefu wako?

a. Kama jibu ni “ndiyo,” je, ni muhimu kiasi gani kugandamiza Mathayo 6:34 kwenye hisia zetu!

I. Rafiki, inaonekana kuwa suluhisho la wasiwasi ni kumwamini Mungu. Anaweza asitatue tatizo katika kipindi cha maisha yetu, anaweza sifanye vitu kwa namna ambayo tungependa afanye, lakini kama tukiamua kuamini maamuzi yake, kama tukifanya kazi kuuendeleza Ufalme wake, hatuhitajiki kudhoofishwa kabisa na wasiwasi. Je, utadhamiria kumwamini Mungu?

IV. Juma Lijalo: Msongo.

0 comments:

Post a Comment